• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa zaidi ya bilioni 12 kujenga vituo vya kutolea huduma za afya Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: September 21st, 2020

SERIKALI ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imetoa fedha kiasi cha Tsh 12,854,209,081 kwa ajili ya kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya 25 na nyumba za watumishi kwenye Halmashauri zote n za Mkoa wa Ruvuma.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema Serikali ya Dkt.John Magufuli  pia imeongeza upatikanaji wa dawa katika Mkoa wa Ruvuma  kwa  kuongeza fedha kutoka Tsh 883,303,792 mwaka 2015 hadi kufikia Tshs. 4,545,139,214 mwaka 2020  ambapo upatikanaji wa dawa umeongezeka kutoka asilimia   51 mwaka 2015 hadi  asilimia 96 mwaka 2020.

"Mkoa wetu unaendelea na mapambano katika kukabiliana na tatizo la Kupunguza maambukizi ya UKIMWI ambapo hadi kufikia mwaka 2020, maambukizi ya UKIMWI yamepungua hadi kufikia  asilimia 5.6 kutoka asilimia 7 mwaka 2015'',alisema.

Kwa mujibu wa Mndeme,Idadi ya vifo vya akina mama wajawazito vimepungua kutoka vifo 46 mwaka 2015 hadi vifo 19 mwaka 2020 na kwamba  kupungua huko kumetokana na uanzishwaji wa huduma za dharura za upasuaji katika vituo vya afya vilivyoboreshwa kwa utekelezaji wa mpango wa “Tuwavushe Salama” ulioasisiwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesema hali ya vifo vya watoto chini ya miaka 5 katika mkoa wa Ruvuma vimepungua hadi kufikia 5/1000 ukilinganishwa na vifo 12/1000 mwaka 2015 na kwamba  vifo vya watoto chini ya mwaka mmoja  vimepungua kutoka vifo 9/1000 mwaka 2015 hadi vifo 3/1000   mwaka 2020 na kutaja hali hiyo inatokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika chini ya uongozi wa Mh. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika sekta ya afya.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 21,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.