• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa zaidi ya bilioni sita kutekeleza mradi wa daraja linalounganisha mikoa ya Ruvuma na Njombe

Imewekwa kuanzia tarehe: August 24th, 2020

SERIKALI ya awamu ya tano inatekeleza mradi wa ujenzi wa daraja la Ruhuhu lenye urefu meta 98.01 linalounganisha Mkoa wa Ruvuma na Njombe kwa gharama ya shilingi bilioni 6.172.

Mradi huo ambao ujenzi wake umechukua muda mrefu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya mafuriko ya mto Ruhuhu unamwaga maji yake ziwa Nyasa.

 Meneja wa Wakala wa Barabara TANROADS mkoani Ruvuma Mhandisi Lazeck Alinanuswe anasema ujenzi umefikia zaidi ya  asilimia 85 ambapo nguzo tatu kati ya nne zilizojengwa ndani ya mto Ruhuhu zimekamilika.

“Ni kweli mradi umechukua muda mrefu, wakati wa mvua za masika mradi ulisimama kutokana na mafuriko ya mto Ruhuhu na baada ya Mvua kupungua mkandarasi ameendelea  kukamilisha kazi ya kujenga nguzo moja sehemu iliyobakia’’,anasema Mhandisi Alinanuswe.

 Mkataba wa ujenzi wa nguzo  nne za daraja  ulisainiwa mwaka 2016 kati ya Mkandarasi wa Kampuni ya M/s Lukolo na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa gharama ya sh bilioni 6.17 na muda wa utekelezaji ni miezi 24.

 Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anasema mradi huo umekuwa unamnyima usingizi kwa kuchelewa kukamilika na kwamba mradi umechukua mrefu kukamilika hasa katika kipindi cha mvua za masika ambapo mto Ruhuhu unafurika na kusababisha   Mkandarasi kushindwa kuendelea na kazi.

“Kazi inayoendelea na Mkandarasi ya kumalizia nguzo moja ambayo inatakiwa kujengwa katikati ya mto Ruhuhu,haiwezi kuendelea wakati mto umefurika,hivyo ujenzi umeanza baada ya mvua kupungua’’,anasema Mndeme.

Anabainisha zaidi kuwa Mkandarasi akishamaliza kazi ya kujenga nguzo moja iliyobakia,ndipo kazi ya kutandaza vyuma na nondo juu ya daraja kupitia nguzo nne itafanywa na TANROADS wenyewe.

“Namuomba Mkandarasi wa daraja hili kufanya kazi hiyo kwa kasi ,ufanisi na ubora ili wananchi wa wilaya za Nyasa mkoani Ruvuma na Ludewa mkoani Njombe waanze kunufaika kupitia daraja hili’’,anasisitiza Mndeme.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 24,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.