• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SIPO tayari kuona Mkoa unafanya vibaya katika sekta ya elimu-RC Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: January 22nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewaagiza wakuu wa shule za  msingi na sekondari kuhakikisha wanainua  kiwango cha ufaulu kwa  wanafunzi  na kuunasua Mkoa kwenye ufauli usioridhisha ambao umedumu kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kanali Thomas ametoa agizo hilo  wakati anazungumza kwenye kikao kazi  na walimu wakuu  wa shule za msingi na wakuu wa shule za sekondari  kilichofanyika kwa nyakati tofauti kwenye ukumbi wa sekondari ya Songea.

“Mtambue kuwa sisi viongozi wenu hatupo tayari kuuona Mkoa unaendelea kufanya vibaya katika sekta ya elimu,hivyo tumieni kikao hiki kuwa chachu ya kufanya mabadiliko,mwaka huu tuanze kwa kufanya mabadiliko makubwa katika utendaji wetu wa kazi ’’,alisisitiza RC Thomas.

Ametahadharisha baada ya kikao hicho hatasikiliza kisingizio chochote kwa matokeo yasiyoridhisha kwenye mitihani ya kitaifa ambapo amewaagiza wakuu hao kujirekebisha na kufanya tathmini ya utendaji kazi ili kuongeza uwajibikaji.

Ili kuhakikisha ufaulu katika elimu ya msingi na sekondari unaongezeka Mkuu wa Mkoa amewaagiza wakuu wa shule kusimamia na kuinua taaluma katika shule zao.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza miradi ya ujenzi kusimamiwa ipasavyo na kusimamia fedha za serikali zinazotolewa kwa uendeshaji wa shule.

Maagizo mengine ambayo ameyatoa ni kila shule kupanda miti ya matunda,kushirikiana na jamii katika kuleta maendeleo ya shule,kuboresha mazingira ya shule,kujiepusha na mikopo inayotolewa na Taasisi zisizo za kibenki na kutekeleza agizo la kila shule kulima hekari tano za mazao ya nafaka,mbogamboga na matunda.

Awali akitoa taarifa ya elimu ya msingi na sekondari kwenye kikao hicho,Afisa Elimu wa Mkoa wa Ruvuma Mwl,Edith Mpinzile amesema Mkoa umeendelea kufanya vibaya kwenye matokeo ya mtihani wa kitaifa kwa kuwa Mkoa umeshindwa kufikia lengo la ufaulu lililowekwa kitaifa la asilimia 85 kwa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi na asilimia 100 ya upimaji wa mitihani ya darasa la nne.

Ameutaja ufaulu wa darasa la saba mwaka 2023 ulikuwa ni asilimia 69.9 na ufaulu wa darasa la nne ni asilimia 76.01 ambapo amesema Mkoa pia umeendelea kufanya vibaya katika mitihani ya sekondari  ya kitaifa kwa kuwa Mkoa umeshindwa kufikia lengo la ufaulu la asilimia 100 kwa mtihani wa upimaji wa kidato cha pili ambapo ufaulu wa Mkoa mwaka 2023 ulikuwa ni asilimia 81.96.

Hata hivyo amesema Idara ya Elimu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imebaini mambo mbalimbali yanayosababisha ufaulu usioridhisha ambayo ameyataja kuwa ni baadhi ya walimu wanashindwa kutekeleza majukumu yao ya kila siku,mada hazikamilishwi na walimu hawatoi mazoezi na majaribio ya kutosha.

Changamoto nyingine amezitaja kuwa ni baadhi ya walimu hawazungumzi na wanafunzi kujua changamoto zao,walimu hawakai kwenye vituo vya kazi,walimu hawana ubunifu na walimu kuwa na madeni yaliyopitiliza ambayo yanaondoa utulivu kazini hivyo walimu wanashindwa kufundisha kikamilifu.

Mkoa wa Ruvuma una shule za msingi  841 na shule za sekondari 233

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.