• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAMASHA kubwa la Toyota kufanyika Ruvuma Novemba 22,2024

Imewekwa kuanzia tarehe: October 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed, ametangaza tamasha la Ruvuma Toyota 2024 litakalofanyika Novemba 22 na 23 mwaka huu ambalo linalenga kuwahamasisha wananchi kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa, utalii, uwekezaji na burudani.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Huntclub mjini Songea Kanali Ahmed Ameyataja malengo ya tamasha hilo ni kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kuufungua Mkoa katika sekta za utalili na uwekezaji na kuleta burudani.

"Tamasha la Toyota Festival 2024 kama Mkoa tumeliandaa kuhamasisha kuelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa ili wananchi wajitokeze kwa wingi, kuendeleza jitihada za kuufungua Mkoa katika sekta za utalii na uwekezaji na kuleta burudani kwa wanaruvuma na mikoa jirani ambayo watapata fursa ya kushiriki," alisema Kanali Ahmed.

Amesema kuwa tamasha hilo litazinduliwa Novemba 22 kwa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo maeneo ya jirani ndani ya Mkoa wa Ruvuma na kuhitimishwa Mbambabay wilayani Nyasa Novemba 23, ambapo kutakuwa na michezo mbalimbali ikiwemo kuogelea, kuvuta kamba, muziki na ngoma za asili.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, amesema kuwa tamasha hilo litakuwa na manufaa kiuchumi na kijamii kwa Mkoa wa Ruvuma, watanzania na mwananchi mmoja mmoja.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Wategi Traders Company, Elizabeth Japheth, amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas kwa jitihada zake katika kuandaa Ruvuma Toyota Festival 2024 na ameikaribisha mikoa jirani kushiriki kwa kuwa lengo ni kuvitangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana Mkoani Ruvuma.

Tamasha la Toyota 2024 linameandaliwa na Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na Wategi Traders Company, ambalo linalenga  kuhamasisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kukuza utalii na uwekezaji, na kutoa burudani kwa wakazi wa Ruvuma na mikoa jirani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.