• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANZANIA yahitaji uwekezaji zaidi wa mashamba makubwa kufungua ajira kupitia kilimo

Imewekwa kuanzia tarehe: May 7th, 2025

Tanzania inahitaji uwekezaji zaidi wa mashamba makubwa ya kilimo ili kufungua fursa za ajira kwa wananchi, kukuza uchumi na kuongeza mapato ya fedha za kigeni kupitia mauzo ya mazao nje ya nchi. Mfano bora wa mafanikio hayo ni Shamba la Kahawa la Aviv Tanzania Limited lililopo Kijiji cha Lipokela, Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma, ambalo limeajiri maelfu ya Watanzania na kuongeza mchango wa zao la kahawa katika uchumi wa Taifa.

Shamba la Aviv lina ukubwa wa zaidi ya hekta 2,000 na huzalisha kahawa bora inayoitangaza Tanzania kimataifa. Meneja wa shamba hilo Hamza Kassim amesema Aviv inachangia asilimia 4.5 ya kahawa yote inayozalishwa nchini, huku asilimia 60 ya kahawa hiyo ikiuzwa moja kwa moja nje ya nchi. Aidha, shamba hilo limeanza kuzalisha pilipili manga kwa mauzo ya nje, hatua inayoongeza mapato ya fedha za kigeni.

Kwa mujibu wa Meneja Msaidizi wa Kampuni hiyo, Muthana Maruvanda, Aviv imewekeza katika miundombinu bora ya umwagiliaji ambayo imekuwa chachu kwa wakulima wa Ruvuma kujifunza kilimo cha kisasa, jambo linalowezesha kuimarika kwa uzalishaji na ubora wa kahawa mkoani humo. Aviv pia hutoa ajira za kudumu zaidi ya 1,400 na ajira za msimu zaidi ya 5,000 kila mwaka.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipotembelea shamba hilo Septemba 2024, alisema mafanikio makubwa katika sekta ya kilimo si bahati mbaya bali ni matokeo ya sera bora na juhudi kubwa za Serikali katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na kurudisha masoko ya mazao. Rais Samia alisisitiza umuhimu wa mashamba makubwa kushiriki katika shughuli za kijamii, ikiwemo uchimbaji wa visima kwa ajili ya umwagiliaji.

Takwimu za kitaifa zinaonesha kuwa uzalishaji wa kahawa umeongezeka kutoka tani 60 hadi tani 85, huku mauzo ya zao hilo nje ya nchi yakiingiza dola milioni 250. Serikali inaamini kuwa uwekezaji zaidi wa mashamba kama Aviv utazidi kuinua sekta ya kilimo, kuleta mapinduzi ya kiuchumi na kuondoa changamoto ya ajira kwa vijana nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • BARAZA la wazee la Makumbusho ya majimaji lachagua viongozi wake

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.