• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA Mbinga kutumia milioni 671 kufanya matengenezo barabara ya Mapera-Ilela

Imewekwa kuanzia tarehe: June 1st, 2023

WAKALA wa barabara za mijini na vijijini(Tarura),imetenga kiasi cha Sh.milioni 671 kwa ajili ya kufanya matengenezo ya dharura Barabara ya Mapera,Mikalanga-Ilela iliyoharibika kutokana na mvua za masika.

Meneja wa TARURA wa wilaya ya Mbinga Oscar Mussa  amesema,matengenezo ya barabara hiyo yanafanywa na kampuni ya Ovans Contruction Ltd  ili iweze kupitia  kwa urahisi na wananchi waitumie katika shughuli zao za usafiri na usafirishaji.

Amesema,mradi huo ni matengenezo ya haraka(dharura) ulianza mwezi Machi na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2023 na kazi zinazofanyika ni ujenzi wa madaraja manne yakiwemo mawili yenye ukubwa wa mita  10,moja la 16 na lingine la mita 5.

Alitaja kazi nyingine zinazofanyika,ni kuchonga barabara wastani wa kilomita 16.96,kuweka kifusi na  kutengeneza mifereji ya maji urefu wa kilomita mita 3.

Baadhi ya watumiaji wa barabara hiyo,wameiomba Serikali kuipatia fedha za kutosha Tarura ili iweze kujenga barabara za vijijini  kwa kiwango cha lami badala ya kujengwa kwa udongo ili ziweze kupitika majira yote ya mwaka.

Solanus Ndomba mkazi wa kijiji cha Maguu amesema,wakati umefika kwa serikali kupitia wizara ya  Tamisemi kuitengea Tarura fedha nyingi ili iweze kuwa na nguvu kubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara zake ambazo kwa muda mrefu zimesahaulika.

Amesema,barabara za vijijini zina mchango mkubwa kiuchumi  kwani zinatumika kusafirisha mazao kutoka shambani kwenda sokoni,hivyo ni muhimu serikali ikaangalia namna ya kutengeneza barabara hizo kwa lami.

Coster Komba mkazi wa kijiji cha Ugano amesema, mbali ya kusafirisha mazao na bidhaa mbalimbali pia barabara hizo zitasaidia sana kuepuka usumbufu kwa wagonjwa wanaohitajika kuwahishwa katika vituo vya Afya na Hospitali kupata matibabu.

Amesema,wakati wa masika barabara hiyo ni changamoto sana kutokana na mvua zinazonyesha, hali inayolazimu kujifunga na hivyo wananchi kukosa mawasiliano kutoka upande mmoja kwenda mwingine.

Ameishukuru serikali kwa uamuzi wa kufanya matengenezo ya barabara hiyo ambayo ni muhimu na mhimili mkubwa wa uchumi kwa wananchi wa Bonde  maarufu la Hagati na wilaya ya Mbinga.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.