• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA walivyofanikiwa kufungua barabara za vijijini Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: March 7th, 2023

WAKALA wa barabara za vijijini na mijini Tanzania(TARURA)wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,imeanza kuzifungua barabara za kimkakati kwenye maeneo yenye shughuli za uzalishaji ili kuharakisha maendeleo katika maeneo hayo na wilaya ya Namtumbo.

Meneja wa Tarura wilayani Namtumbo Mhandisi Fabian Lugalaba amesema, barabara hizo zitawasaidia wakulima  kusafirisha mazao yao kutoka shambani hadi sokoni,kupata bei nzuri na kukomesha tabia ya wafanyabiashara wanaokwenda mashambani kununua mazao kwa bei ndogo isiyolingana na gharama za uzalishaji.

Lugalaba alisema,kwa fedha 2022/2023 wakala wa barabara za vijijini na mijini(Tarura) imetumia zaidi ya shilingi milioni 40 kufanya matengenezo ya barabara mpya mbili ya Minazini-Muungano na Barabara ya Mtonya-Irrigation yenye urefu wa kilomita 14 ambapo alieleza kuwa,kukamilika kwa barabara hiyo na nyingine zinazoendelea kujengwa wilayani humo ni mafanikio makubwa tangu serikali ya awamu ya pili ilipoingia  madarakani.

Lugalaba ameeleza kuwa,sehemu kubwa ya barabara hizo zimepita kwenye maeneo ambayo wananchi wake wamejikita zaidi na kilimo cha umwagiliaji ambacho kina mchango mkubwa wa kiuchumi kutokana na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara ikiwemo kahawa,mahindi na mpunga.

Kwa mujibu wa Lugalaba ni kwamba,tangu Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na sasa Tanzania maeneo hayo hayakuwa na barabara kabisa ambapo wakulima walilazimika kusafirisha mazao yao kwa ubeba kichwani,jambo lililowaathiri sana katika jitihada zao za kujikwamua na umaskini.

Alisema,serikali ya awamu ya sita  kupitia fedha za tozo imetambua umuhimu  na shughuli zinazofanyika katika maeneo hayo,imefanya matengenezo ya kuzifungua barabara hizo ambazo kwa sasa zimekamilika na zimeanza kupitika.

Baadhi ya wananchi wanaofanya shughuli za kilimo katika maeneo hayo wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassa na serikali yake ya awamu ya sita kwa kutoa fedha zilizotumika kuzifungua barabara hizo ambazo zinakwenda kuchochea maendeleo na uchumi wao.

Babu Ponera alisema,hapo awali wananchi hususani wakulima wa maeneo hayo walipata shida kubwa ya kubeba mbolea kichwani kutoka kijijini kupeleka shambani,jambo ambalo lilisababisha wakulima wengi kutofikia malengo ya uzalishaji.

Ponera,ameipongeza serikali kwa kuifungua barabara hiyo ambayo ni muhimu kwa uchumi wa wilaya ya Namtumbo kutokana na maeneo hayo kuwa yenye uzalishaji mkubwa wa mazao katika wilaya ya Namtumbo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.