• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TRA yawashukuru wahariri kuhamasisha wananchi kulipa kodi

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2025

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo, amewashukuru viongozi na wanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kwa kuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya TRA katika kuhamasisha umma kuhusu ulipaji wa kodi.

Akizungumza katika mkutano mkuu maalum wa siku mbili wa TEF uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Bombambili, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Kayombo amesema kuwa TRA inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa wahariri na vyombo vya habari katika kufikisha ujumbe wa kodi kwa wananchi kwa lugha nyepesi na inayoeleweka.

Kayombo amesema, mafanikio ya kuvuka lengo la ukusanyaji wa kodi hayawezi kutenganishwa na kazi kubwa inayofanywa na wahariri na wanahabari kwa ujumla. “Sisi na ninyi tunajenga nyumba moja ya maendeleo, mnapotumia majukwaa yenu kuelimisha, kuhamasisha, na kuhimiza wananchi kudai risiti na kulipa kodi, mnafanya kazi ya kubwa na tunathamini mchango wenu”, amesema Kayombo.

Aidha, Kayombo amewapongeza viongozi wapya wa TEF waliochaguliwa ma kueleza kuwa uchaguzi huo umekua mfano bora wa demokrasia na weledi na kuufanya kuwa uchaguzi huru na wenye haki.

Naye Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma, Nikodemas Mwakilembe amewapongeza wahariri kwa uchaguzi huru na wenye kuzingatia misingi ya uchaguzi na utulivu wa hali ya juu na kuongeza kuwa uongozi huo unaimarisha imani ya wadau kwa TEF na kuchochea ushirikiano mzuri baina ya vyombo vya habari na taasisi za serikali kama TRA.

TRA imeahidi kuendeleza ushirikiano wake na wanahabari kwa lengo la kufanikisha elimu ya ulipaji kodi na kuongeza makusanyo ya mapato ya serikali.

Kwa upande wake, Mwenyekiti mpya wa TEF aliyechaguliwa Deodatus Balile ameipongeza TRA kwa kushirikiano wa wakati wote na kuahidi kuendelea kuwa daraja kati ya mamlaka na wananchi kwa kuwafikia walipakodi kupitia vyombo vya habari.

Mkutano Mkuu Maalum wa TEF ulifunguliwa rasmi na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi na kuhudhuriwa na wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, na ulihusu masuala muhimu yanayogusa uhuru wa vyombo vya habari, maadili ya taaluma hiyo, na nafasi ya wahariri katika kuchochea maendeleo ya nchi kupitia uandishi wa habari za kuelimisha.

TRA imekuwa ikishirikiana na wahariri kwa njia mbalimbali ikiwemo warsha za pamoja, mafunzo ya uandishi wa habari za kodi, usambazaji wa taarifa kwa wakati, pamoja na kudhamini mikutano ya TEF kama huu wa Songea. Ushirikiano huu umelenga kujenga uelewa mpana wa masuala ya kodi miongoni mwa wanahabari ili waweze kutoa taarifa zenye weledi, usahihi, na ushawishi kwa jamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.