• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU kujenga ofisi ya kisasa kwa kila kijiji

Imewekwa kuanzia tarehe: May 18th, 2023

HALMASHAURI ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,imeanza kujenga ofisi za kisasa kwa kila kijiji zitakazotumika kutoa huduma bora kwa wananchi na kupanua wigo wa kuongeza mapato ya Halmashauri na Serikali kwa ujumla.

Hayo yamesemwa  na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Hairu Musa,alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa  mradi wa ofisi ya kijiji cha Tuleane kata ya Mchangani ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 95.

Alisema,wilaya Tunduru ina vijiji 157 ambavyo vinakwenda kupata ofisi za kisasa kwa ajili ya maafisa watendaji ambao watashirikiana na watumishi wengine wa Halmashauri kukusanya mapato ya ndani kwa asilimia 100.

Alisema,katika mkakati wao wa kukusanya na kuongeza mapato ya ndani,wameanza kuboresha maeneo ya kazi ambayo yatakuwa rafiki,kuchochea ari ya kazi na uwajibikaji kwa watumishi.

Kwa mujibu wa Hairu ni kwamba,hatua  hiyo itasaidia sana Halmashauri kuwa na uwezo wa kujiendesha na kutoa huduma bora za kijamii, badala ya kutegemea mapato kutoka Serikali kuu.

Hairu ambaye ni Diwani wa kata ya Mchangani alisema,kata yake ina vijiji vitano,kati ya hivyo vijiji vitatu wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri wamekamilisha ujenzi wa ofisi na matarajio yao ifikapo mwaka 2025 vijiji vilivyobaki vipate ofisi mpya.

Hairu amewataka viongozi kuanzia ngazi za vijiji na kata,kuwashirikisha wananchi katika maeneo yao kuibua miradi  mbalimbali ikiwemo ujenzi wa zahanati,vituo vya afya,miradi ya maji ,miundombinu ya barabara na ofisi za vijiji ili kuharakisha maendeleo na kukuza uchumi.

Amewaomba wadau wakiwemo wafanyabiashara,madiwani na wabunge wa Jimbo la Tunduru Kusini na Kaskazini,kuunga mkono kwa kuchangia ujenzi wa ofisi za vijiji ambazo ni chanzo mojawapo cha mapato.

Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Tuleane Said Goloka alisema,awali walilazimika kutumia nyumba ya mwananchi kuendesha shughuli zao,hata hivyo changamoto  kubwa ilikuwa kipindi cha masika kwani nyumba hiyo ilikuwa mbovu.

Alisema,hali hiyo iliwalazimu watumishi wa serikali ngazi ya kijiji kutoka nje kila inaponyesha mvua ili kukwepa kuangukiwa na paa la nyumba kutokana na uchakavu wake.

Goloka,ameipongeza serikali kupitia Halmashauri ya wilaya kuanzisha ujenzi wa ofisi mpya za kijiji na kueleza kuwa ,zitasaidia kuchochea  maendeleo na kuhamasisha wananchi kupenda kushiriki na kujitolea nguvu zao katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.