• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UBORESHAJI Daftari la wapigakura kuanza Januari 12 Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: January 1st, 2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka wadau wa uchaguzi mkoani Ruvuma kutumia nafasi zao katika jamii kuwafikishia wanaruvuma taarifa sahihi na kwa wakati zinazohusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Daftari na TEHAMA wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Stanslaus Mwita, wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele kwenye mkutano wa Tume na wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura uliofanyika katika ukumbi wa Chandamali mjini Songea mkoani Ruvuma.

"Kufanikiwa kwa zoezi hili la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Mkoa wa Ruvuma, kunategemea sana ushiriki wenu katika kutoa elimu na kuhamasisha wananchi wenye sifa wajitokeze kwa wingi kandikishwa au kuhamisha au kuboresha taarifa zao," alisema Mwita.

Amebainisha kuwa katika mkoa wa Ruvuma zoezi hilo litafanyika kwa muda wa siku 7 kuanzia Januari 12 hadi 18, 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, Mbinga, Mbinga Mji, Wilaya ya Songea na Manispaa ya Songea ambapo vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi hadi 12:00 jioni.

Katika hatua nyingine Mwita amewakumbusha wadau na wananchi kuwa kadi zilizotolewa mwaka 2015 na 2020 zenye jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni halali na zitaendelea kutumika katika chaguzi zijazo, hivyo zoezi hilo la uboreshaji wa Daftari halitawahusu wapiga kura wenye kadi hizo, na ambao kadi zao hazijaharibika, kupotea au hawajahama kutoka eneo moja la uchaguzi kwenda eneo jingine au taarifa zao hazijakosewa au hawahitaji kuboresha taarifa zao.

Naye Mratibu wa Uandikishaji Mkoa wa Ruvuma, Salum Kateula, amesema mkoa wa Ruvuma utakuwa na awamu mbili za Uandikishaji ambapo awamu ya kwanza itahusisha halmashauri tano ikiwemo Songea MC, Songea DC, Mbinga DC, Mbinga TC na Nyasa DC ambapo uboreshaji huo wa Daftari utaanza Januari 12 hadi 18, 2025, na awamu ya pili itajumuisha Halmashauri tatu ambazo ni Namtumbo DC, Tunduru DC na Madaba DC ambapo zoezi hilo litaanza Januari 28 hadi Februari 3.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ni zoezi muhimu linalofanyika ili kuhakikisha taarifa za wapiga kura ziko sahihi ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi Mkuu utakaofanyika  mwaka 2025, kauli mbiu ya zoezi hili ni "Kujiandikisha Kupiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora."

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.