• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI madarasa 156 ya sekondari wakamilika Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 30th, 2022

SERIKALI mkoani Ruvuma imekamilisha mradi wa ujenzi wa madarasa 156 pamoja na samani zake katika shule za sekondari yaliyogharimu shilingi bilioni 3.1. 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mwezi Oktoba mwaka huu ilitoa fedha za kutekeleza mradi huo mkoani Ruvuma. 

“Madarasa yapo tayari kupokea wanafunzi waliochaguliwa kidato cha kwanza Januari 2023”,alisisitiza RC Thomas. 

Hata hivyo amesema hayo ni mafanikio makubwa kwa kuwa sasa katika Mkoa mzima shule zote za sekondari za Serikali zina uhakika wa kupokea wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule hizo.

Amesema hakuna kikwazo tena cha uhaba wa vyumba vya madarasa hivyo ametoa rai kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wanaripoti bila kukosa. 

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi bilioni 7.7 zilizojenga shule mpya za sekondari 11 mkoani Ruvuma katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022. Amesema uboreshaji wa miundombinu ya elimu umepunguza utoro na kuongeza ufaulu. 

Ametolea mfano ufaulu wa mitihani ya Taifa ya kidato cha nne mwaka 2021 Mkoa ulikuwa na ufaulu wa asilimia 90.1.

Kulingana na RC Thomas matokeo ya mitihani ya Taifa ya kidato cha sita mwaka 2022 Mkoa wa Ruvuma umefaulisha kwa asilimia 99.9. 

Hata hivyo amesema jitihada zinafanyika kuboresha ufaulu wa darasa la saba na kidato cha nne.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.