• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI wa barabara ya Mbinga -Mbambabay wakamilika kwa asilimia 100

Imewekwa kuanzia tarehe: February 22nd, 2022

UJENZI wa Barabara ya Mbinga –Mbambabay mkoani Ruvuma yenye urefu wa kilomita 66 iliyojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya Chico kwa gharama ya Sh.bilioni 129,361,352,517.84 imekamilika na kuanza kutumika.

Mhandisi Mwandamizi wa miradi kutoka ofisi ya wakala wa Barabara nchini(Tanroads)mkoa wa Ruvuma Justine Mrope alisema, ujenzi wa barabara hiyo ulianza mwezi April 2018 na kukamilika rasmi mwezi Januari 2021.

Mrope alisema,kukamilika kwa Barabara hiyo kutaleta maendeleo makubwa katika wilaya ya Mbinga,Nyasa na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla kwa kuwa wakulima wengi wataweza kusafirisha mazao na bidhaa mbalimbali.

Alisema, mradi huo wa barabara ya Mbinga-Mbambabay unajumuisha na ujenzi wa mizani katika eneo la Buluma ambayo imekamilika kwa ajili ya kusaidia kudhibiti uzito wa magari,hata hivyo haijaanza kutumika kutokana na kukosa watumishi.

Kwa mujibu wa Mrope, kabla ya barabara ya Mbinga-Mbambabay kujengwa kulikuwa na changamoto nyingi ikiwamo baadhi ya akima mama wajawazito kujifungulia njia kabla ya kufika zahanati na vituo vya afya kutokana na umbali na ubovu wa barabara,lakini sasa changamoto zimemalizika.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Tanroads mkoa wa Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutoa fedha ambazo zimewezesha kumaliza ujenzi wa barabara hiyo ambayo inakwenda kuchochea kukua kwa uchumi wa wananchi wa wilaya hizo.

“kwa kweli napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru sana Rais Samia Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha ili kuendelea na kazi za matengenezo ya barabara,ujenzi na ukarabati wa barabara ,makalavati na madaraja katika mkoa wetu” alisema.

Aidha alisema, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Tanroads mkoa wa Ruvuma imeidhinishiwa jumla ya Sh.bilioni 23.742 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na madaraja.

Mlavi alisema,Tanroads mkoa wa Ruvuma inalo jukumu la kusimamia matengenezo ya mtandao wa Barabara wenye urefu wa kilometa 2,166.62 kati ya hizo Barabara kuu zina urefu wa kilometa 920.98 na Barabara za mkoa zina urefu wa kilometa 1,245.65.

Alisema, kati ya kilometa 920.98 za Barabara kuu,kilometa 702.60 ni za lami na kilometa 218.38 ni changarawe na wanaendelea kufanya kazi za matengenezo ya barabara,ujenzi na ukarabati wa barabara na madaraja, na usimamizi wa hifadhi za barabara na mizani.

Alisema, hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Disemba 2021 jumla ya mikataba 47 imesainiwa na matengenezo ya barabara kuu na barabara za mikoa yalikamilika kwa asilimia 57 za utekelezaji wake.

Mkazi wa wilaya ya Mbinga John Millanzi,ameipongeza wizara ya ujenzi kwa kumaliza changamoto ya barabara na Tanroads kwa usimamizi mzuri ambao umefanikisha kujengwa kwa viwango na kukamilika kwa muda uliopangwa.
MWISHO

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.