• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UTALII wa utamaduni;Chifu wa wangoni alivyozikwa Songea na watu wawili wakiwa hai mwaka 1889

Imewekwa kuanzia tarehe: March 8th, 2021

MOJA ya vivutio vya utalii wa kiutamaduni vinavyopatikana katika kijiji cha Mbingamharule wilaya ya Songea mkoani Ruvuma ni uwepo wa kaburi la duara ambalo Chifu Nkosi Mharule bin Zulu Gama alizikwa mwaka 1889.

 Mambo ambayo yanawashangaza wengi wanaotembelea kaburi hili ni historia inayoonesha kuwa Nkosi Mharule baada ya kufariki alizikwa kwa desturi na mila za kichifu za kabila la wangoni toka Afrika ya kusini.

 Christian Ngonyani mwenye umri wa miaka 87 ni mzee wa Mila katika kijiji cha Mbingamharule anasema kijiji hicho kimepewa jina la chifu huyo ambaye alitokea nchini Afrika ya kusini na kutawala ungoni kuanzia mwaka 1847 hadi 1889 alipofariki na kuzikwa katika kijiji hicho.

“Chifu Mharule  baada ya kufa mwaka 1889 alizikwa kwa taratibu za jadi ya machifu wa Afrika ya kusini,kaburi lake lilikuwa la mviringo,sanda yake ilikuwa ya ngozi ,alikarishwa kwenye kiti cha ngozi,walikamatwa watu wawili wakiwa hai walizikwa naye wakiwa wamesimama mbele na nyuma ya chifu’’,alisimulia mzee Ngonyani.

Amezitaja taratibu za kijadi za wakati huo zilitaka Mfalme au Chifu anapofariki ni lazima azikwe na watu wawili wakiwa hai na kusisitiza kuwa hiyo ilikuwa ni amri ya serikali ya jadi na hapakuwepo mtu aliyepinga.

 Mzee Ngonyani amewataja wengi waliokuwa wanazikwa wakiwa hai na Mfalme ni wale ambao walikuwa wamezoeana na kufanyakazi naye kwa karibu.

Hata hivyo amesema kaburi hilo linatumiwa na wananchi wa kijiji hicho kwenda kuhiji kila mwaka kwenye kaburi hilo ambalo lipo kilometa mbili toka kijijini hapo na kwamba ndugu wa Chifu Mharule toka Afrika ya Kusini huwa wanafika kufanya matambiko kwenye kaburi hilo.

Amesema mwaka juzi ukoo wa Mharule toka Afrika ya kusini walifika kushuhudia kusimikwa kwa Chifu Nkosi Imanuel Zulu Gama wa Tano ambaye ndiyo chifu wa wangoni wa sasa.

Amesema yeyote ambaye anapenda kwenda kutembelea kaburi hilo kuna taratibu zake za kimila ambazo amezitaja kuwa ni kubeba unga wa muhogo,mahindi na ulezi ambao unatengenezwa na bibi katika kijiji hicho.

Baada ya kufika eneo la kaburi anatangulia mhusika ambaye anawasiliana na chifu kwa lugha ya jadi ndipo wanaoitwa waliofika kutambika na kupiga magoti juu ya kaburi na kuomboleza kwa sala za jadi.

“Baada ya maombi kuku au mbuzi wanachinjwa juu ya kaburi la  Chifu Mharule,jambo la kushangaza mbuzi anapochinjwa hapigi kelele,baada ya kuchinja mmoja anamwaga unga  wote juu ya kaburi’’,anasema.

Hata hivyo anasema ukifika asubuhi juu ya kaburi hauoni damu wala unga vyote vinakuwa vimeliwa na kwamba hiyo ndiyo ishara ya kukubaliwa shida zote ambazo ulikwenda kuomba kwenye kaburi hilo.

Agnes Ngonyani Msaidizi wa Mzee Ngonyani  amesema  wanapokea wageni wengi wanaotembelea kaburi la Chifu Mharule kutoka nchi za Ulaya,Marekani na Afrika ambao wanakwenda kwa shida mbalimbali ikiwemo kuhiji na kufanya matambiko.

“Nimekuwa nawapeleka watu wa kawaida,waganga wa jadi,watalii na wagonjwa wanaenda kufanya maombi kwenye kaburi la Chifu na kufanikiwa’’,anasema Ngonyani.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 8,2021

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.