• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UZINDUZI kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kufanyika Ruvuma Julai 22

Imewekwa kuanzia tarehe: June 12th, 2023

MKOA wa Ruvuma unatarajia kuzindua kampeni ya kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) Julai 22 mwaka huu katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Mwenyekiti wa Kampeni hiyo katika Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki ambaye pia ni Katibu TawalaMkoa wa Ruvuma,amesema mara baada ya uzinduzi wa kitaifa,kampeni hiyo inatarajia kufanyika kwa siku kumi kisha kuendelea hadi Desemba 2023.

Hata hivyo amesema kampeni hiyo inatarajia kufanyika katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma ambapo kila Halmashauri kampeni itafanyika katika kata kumi  na kwamba katika kila Kata kampeni itafanyika katika vijiji vitatu.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Songea mjini Dkt.Damas Ndumbaro ameitaja Kampeni ya Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kuwa inalenga kulinda na kukuza haki ya upatikanaji haki kupitia huduma za msaada wa kisheria nchini’’,alisisitiza.

“Kampeni inatarajia kuboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza hususan wanawake,Watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu,kampeni itachangia kuimarisha amani na utulivu na kuleta utengamano wa kitaifa’’,alisisitiza.

Dkt.Ndumbaro amesema kampeni hiyo inatarajia kufanyika kwa miaka mitatu kuanzia Machi 2023 hadi Februari 2026 na kwamba kampeni inafanyika katika nchi nzima kwenye mikoa yote Tanzania bara na Zanzibar kwa kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi.

Amebainisha zaidi kuwa elimu ya kisheria italenga katika masuala ya ukatili wa kijinsia,migogoro ya ardhi,mirathi,usuluhishi kwa njia  mbadala,mifumo ya kisheria na masuala yahusuyo haki za binadamu kwa ujumla.

“Ni matarajio yangu kwamba wadau wote wa huduma ya msaada wa sheria nchini watashiriki ipasavyo katika kutekeleza shughuli za kampeni hii ambayo itaboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza na kupunguza matukio ya udhalilishaji wa kijinsia na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini’’,alisisitiza Ndumbaro.

Kumekuwa na ongezeko la wananchi waliopata huduma ya msaada wa kisheria hapa nchini ambapo takwimu za hivi karibuni zinaonesha  katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2022,jumla ya watu 41,924 walipatiwa huduma ya msaada wa kisheria kati yao wanaume 17,068 na wanawake 24,856.

Pichani ni Mwenyekiti  wa Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 12,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.