• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIJIJI Ruvuma kuingizwa kwenye mpango wa usimamizi wa kudhibiti matukio ya moto

Imewekwa kuanzia tarehe: June 26th, 2024

Wadau wa  maliasili katika Mkoa wa Ruvuma wameazimia  kuweka vijiji vyote kwenye mpango wa usimamizi jumuishi ili kukabiliana changamoto ya moto.

Maazimio hayo yamepitishwa kwenye kikao cha wadau hao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mipango Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea, kilichoongozwa na  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye aliwakilishwa na  Mkuu wa Wilaya ya  Nyasa Mheshimiwa Peres Magiri.

Kikao hicho kimefadhiliwa na Mradi wa Panda miti kibiashara na kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) mameneja wa mashamba ya miti ya serikali,Mwakilishi kutoka Chuo Kikuu cha SUA na wawezeshaji  wa majanga ya moto na usimamizi wa moto vijijini.

Mwezeshaji Andrew Fernand akizungumzia usimamizi wa moto vijijini,amesema mpango huo unatekelezwa katika Halmashauri kumi  hapa nchini katika kipindi cha miaka mitano ambapo ameitaja moja ya Halmashauri hizo ni ya Madaba iliyopo mkoani Ruvuma.

Amesema program hiyo katika  Halmashauri ya Madaba inatekelezwa katika kijiji cha Wino na kwamba ili kutekeleza mpango huo kila Halmashauri itakuwa na Msimamizi wa masuala ya moto.

Hata hivyo amesema mpango wa kupambana na moto katika Halmashauri ya Madaba unatekelezwa katika vijiji saba na kwamba vijiji vyote vimeweka sheria zinazosaidia kukabiliana na majanga ya moto unatokea hasa katika kipindi cha kiangazi.

Amesema kati ya vijiji saba vinavyotekeleza mpango huo ni Kijiji kimoja tu cha Wino ndicho kina mfuko wa fedha wa kupambana na moto na kwamba vijiji vinne kati ya saba vimenunua vifaa vya kupambana na majanga ya moto.

“Chanzo kikuu cha moto ni wakulima wanapoandaa mashamba yao,wananchi wanatakiwa kubadilika kifkra kuhusu kuandaa mashamba kwa kuchoma moto,elimu inatakiwa kuwa endelevu Pamoja na ununuzi wa vifaa vya kukabiliana na moto’’,alisema.

Naye Mwakilishi wa Meneja Hifadhi ya Misitu Wino Madaba   Goffrey Shio amesema shamba hilo limepanda miti Zaidi ya hekta 5000 ya aina mbalimbali na kwamba hifadhi hiyo  katika kipindi cha mwaka  2012 hadi 2024 imeweza kuotesha jumla ya miche milioni 8.8.

Hata hivyo  amesema wakulima wenye mashamba ya mabondeni uandaa mashamba yao kwa kutumia moto na kwamba moto huo kila mwaka umekuwa unaleta madhara makubwa kwa kuunguza mashamba ya miti ya wananchi ambapo mwaka 2023 zaidi ya hekta 3000 za mashamba ya miti ya wananchi ziliteketea kwa moto.

Akizungumza kwenye kikao hicho Kamanda  wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Ruvuma SF Melenia Nyabwinyo ameomba kuimarisha ushirikiano baina ya Idara ya Zimamoto na wadau wa misitu Pamoja na wananchi  kwa kutoa taarifa mapema za matukio ya moto ili kufanya uchunguzi wa moto kwa wakati.

Nyabwinyo ametoa rai kwa  TFS  na wamiliki wa misitu kuwalipa posho zao kwa wakati wafanyakazi wanaojitolea kulinda mashamba ya miti na  misitu yao ili wasiweze kuhujumu kwa kuanzisha moto baada ya kuchelewa kuwalipa maslahi yao.

Akizungumza  wakati anafunga kikao hicho Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Peres Magiri  amesisitiza elimu ya kukabiliana na mto iwe endelevu na itolewe kuanzia ngazi ya vijiji.

Amesisitiza kila Kijiji kianzishe Kamati na vikosi vya kukabiliana na matukio ya moto Pamoja na kutoa mafunzo ya mara kwa mara na ununuzi wa vifaa vya kuzimia moto ili kulinda rasmali za misitu.

“Majukumu ya kuanzisha Kamati za moto za vijiji tumekubaliana kuanzia Julai mwaka huu sanjari na kutoa elimu na namna ya kuunda mfuko wa fedha kwa ajili ya vijiji  kuhusu suala la moto’’,alisisitiza Magiri.

Ametaka kuwashirikisha wadau kuanzia ngazi kamati za vijiji hadi kwenye Wilaya kwenye mpango jumuishi wa vijiji kukabiliana, kudhibiti na kuzuia  majanga ya moto.

Amesisitiza kuwa wadau wa misitu wana kazi kubwa ya kuwaelimisha wananchi vijijini na wadau wote  ili wapate taarifa sahihi katika kudhibiti matukio ya moto.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.