• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIJIJI sita Nyasa kuanza kunufaika na maji ya RUWASA

Imewekwa kuanzia tarehe: January 27th, 2024

WAKALA wa maji na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa)wilaya ya Nyasa,uko hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa mradi wa maji Ngumbo utakaohudumia wakazi 11,080 wa vijiji sita  katika kata ya Ngumbo kwa gharama ya zaidi ya Sh.bilioni 4.6.

Meneja wa Ruwasa wilaya ya Nyasa Mhandisi Masoud Samila,amevitaja vijiji vitakavyonufaika na mradi huo ni  Hinga,Mbuli,Ngumbo,Mkili,Yola na Liwundi.

Kwa mujibu wa Samila,mradi  huo unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo  awamu ya kwanza  umetekelezwa katika kijiji cha Hinga ambacho wananchi wameanza kupata huduma ya maji safi na salama na  fedha zilizotumika ni Sh.bilioni 2.6.

Masoud amezitaja kazi zilizofanyika katika awamu hiyo ni kujenga matenki mawili moja la lita 75,000 na lingine lita 200,000,kujenga chanzo,(Intake),vituo vya kuchotea maji na kulaza bomba za kusambaza maji umbali wa kilomita 23.

Alisema,awamu ya pili inahusisha kazi ya kulaza bomba za kusambaza maji umbali wa kilomita 29.5 na kujenga vituo vya kuchotea maji 30 katika vijiji vitano vilivyobaki kazi itakayogharimu Sh.bilioni 2,030,668,500.

Ametaja kazi zinazofanyika ni kulaza bomba za kusambaza maji urefu wa kilomita 29.5 na ujenzi wa vituo  vya kuchotea maji 30  ambapo ujenzi wake umefikia asilimia  25 na utakamilika  ifikapo mwezi April mwaka huu.

Katika hatua nyingine Samila alisema, wilaya ya Nyasa ina jumla ya vijiji 84 kati ya hivyo vijiji  46 vinapata huduma ya maji ya bomba na vijiji 38 vilivyobaki vinapata huduma ya maji kupitia visima vya asili na vyanzo mbalimbali.

Alisema,katika bajeti ya mwaka 2023/2024 Ruwasa wilaya ya Nyasa ilipanga kukamilisha miradi 6 ambayo ilipangwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na miradi mipya 3

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.