• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VITUO vya kutolea huduma za afya Ruvuma vyafikia 473

Imewekwa kuanzia tarehe: September 21st, 2024

MKOA wa Ruvuma umefanikiwa kuboresha huduma za afya ambapo hivi sasa  vituo vya kutolea  huduma za afya vimeongezeka hadi kufikia 473.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ofisini kwake mjini Songea  wakati wa mapokezi ya Waziri wa Afya Mheshimiwa Jenista Mhagama.

Kanali Abbas  amebainisha kuwa vituo hivyo vya kutolea huduma za afya vinajumuisha hospitali 18,vituo vya afya 50,zahanati 341,kliniki 17 na maabara 47.

Ameongeza kuwa huduma za uchunguzi pia zimeimarika ambapo serikali ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imenunua mashine moja ya CT Scan na Digital X ray 11 na kuzisambaza katika vituo vya kutolea huduma za afya ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

“Hapo awali huduma za CT Scan zilikuwa hazipatikani ndani ya Mkoa wa Ruvuma na huduma za x ray zilikuwa zinapatikana katika Halmashauri ya Tunduru na hospitali ya Mkoa tu’’,alisisitiza.

Ameongeza kuwa katika eneo la miundombinu ya afya kazi kubwa imefanyika  ambapo hadi kufikia mwaka 2023/2024 shilingi bilioni 32.26 zimetolewa na  kwamba katika kipindi hicho hospitali sita za halmashauri zimejengwa ambapo  hadi sasa ujenzi wa hospitali hizo umegharimu shilingi bilioni 16.5  na kwamba serikali imetumia shilingi bilioni 1.8 kukarabati hospitali kongwe.

Akizungumzia mradi wa hospitali ya rufaa ya Mkoa ,Kanali Abbas amesema mradi huo ni mafanikio makubwa ambapo baadhi ya huduma zimeanza kutolewa kwa baadhi ya majengo yaliyokamilika yakiwemo jengo la mionzi lilijengwa kwa shilingi bilioni 2.34.

Majengo mengine ambayo yamekamilika ameyataja kuwa ni jengo la magonjwa ya dharura EMD lililogharimu shilingi milioni 784,ukarabati wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU) kwa gharama ya shilingi milioni 152,jengo la tiba mtandao lililogharimu shilingi milioni 33.1.

Hata hivyo amesema ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje OPD unaendelea ambapo hadi sasa shilingi bilioni 3.36 zimetumika,pia serikali imetoa shilingi milioni 650 kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kuzalisha hewa ya Oksijen na ujenzi wa jengo la huduma ya dialysis unaendelea ambapo jumla ya shilingi milioni 480 zimetolewa na ujenzi umefikia asilimia 78.

Mafanikio mengine ambayo yamepatikana ni katika utoaji wa huduma za afya ya uzazi,mama na mtoto ameyataja kuwa ni wajawazito wanaohudhuria kiliniki wameongezeka na idadi ya wajawazito waliojifungua katika vituo vya afya imeongezeka kutoka asilimia 85 mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 99.2 mwaka 2024.

Akizungumza baada ya kupata taarifa hiyo,Waziri wa Afya Mheshimiwa Jenista Mhagama  amesema serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hivyo kufanikisha kutoka huduma za kibingwa katika hospitali zilizopo ndani ya Mkoa.

Amesema serikali imeweka sheria ya Bima ya afya kwa wote ili kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma ya afya na kwamba serikali imeshaleta fedha nyingine kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje OPD katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

Katika hatua nyingine Waziri Mhagama amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais -TAMISEMI itatoa mafunzo rasmi ya kuwajengea uwezo watoa huduma za Afya ngazi ya jamii 11,515 kuanzia Septemba 30, 2024 ili kufanikisha azma ya Mpango Jumuishi wa wahudumu hao na kuendeleza afua jumuishi za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii.

Waziri Mhagama amesema mpango huo utaanza kwenye Halmashauri 21 ndani ya mikoa 11 katika awamu ya kwanza

“Mikoa ambayo itafikiwa na huduma hii kwa Awamu ya kwanza ni pamoja na Geita, Pwani, Tanga, Songwe, Mbeya, Lindi, Tabora, Kagera, Njombe, Ruvuma, na Kigoma" ameainisha waziri Mhagama na kuongeza kuwa

 Ameutaja mpango huo umelenga na unahitaji kuwa na wahudumu wawili wa jinsia ke na me kila mtaa na kila kitongoji,na kwamba uchaguzi wa wahudumu hao umeshirikisha wananchi na wana jamii kutoka kitongoji husika au mtaa husika

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.