• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WADAU wa maendeleo ya elimu Ruvuma walivyoazimia kuchangia elimu kupitia GPE

Imewekwa kuanzia tarehe: July 28th, 2023

WADAU wa Maendeleo ya elimu mkoani Ruvuma wameazimia kufanya vikao na wadau wa elimu kwa kila Halmashauri ambao wanaweza kutoa ahadi ya kuchangia maendeleo katika sekta ya elimu.

Azimio hilo limetolewa katika kikao cha wadau wa maendeleo ya elimu Mkoa wa Ruvuma kilichohusu kujadili  namna ya kunufaika kupitia Mfuko wa kusaidia maendeleo ya elimu Duniani (GPE) ambacho  kimefanyika kwa siku moja kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mgeni rasmi katika kikao hicho alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile.

Akizungumza kwenye kikao hicho,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote nane kuhakikisha wanafanya vikao vya kukutana na wadau wa maendeleo ya elimu na kuleta taarifa za vikao hivyo Pamoja na orodha ya wadau na kiwango cha fedha na vifaa ambavyo wameahidi kusaidia sekta ya elimu katika Halmashauri husika.

“Taarifa hiyo ifike katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kabla ya Agosti 15 mwaka huu na ofisi ya Mkuu wa Mkoa itajaza taarifa zinazohitajika kiserikali na kuwasilisha Wizara ya Elimu kabla ya Agosti 25,2023 ili Mkoa wa Ruvuma uwe sehemu ya watanzania  watakaonufaika na mradi wa GPE’’,alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Akizungumzia mfuko  wa GPE kwenye kikao hicho,Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Stephen Ndaki  amesema Tanzania ilianza kunufaika na mfuko wa GPE tangu mwaka 2013 na kwamba hadi sasa serikali imenufaika  kwa awamu mbili.

 Amesema awamu ya kwanza ya unufaikaji wa mfuko huo ilianza mwaka 2014 hadi 2018 na awamu ya pili ilianza mwaka 2019 na inatarajia kufikia ukomo Januari 2024.

Hata hivyo amesema  katika ufadhili unaotarajia kuanza mwaka wa fedha 2023/2024,Tanzania imepewa nafasi ya kuomba fedha kupitia aina tatu za ufadhili ambazo amezitaja kuwa ni System capacity Grant (SCG),Sysytem transformation grant (STG) na multilier grant (MG).

“Ndugu wadau wa elimu,mpaka sasa kupitia idhini ya Bodi ya wakurugenzi wa GPE,nchi imenufaika kupitia SCG imepata Dola za Marekani 3,999,000 na kupitia STG nchi imepata Dola za Marekani 84,664,800’’,alisema Ndaki.

Hata hivyo amebainisha kuwa maombi yaliyowasilishwa ili nchi iweze kupata fedha za ufadhili kupitia MG hayajafanikiwa kufikia hatua ya kupata idhini ya Bodi ya wakurugenzi wa GPE.

Amesisitiza kuwa ili kupata fedha ambazo zimefungiwa inahitajika wadau wa elimu kutoa ahadi au mali kauli kuonesha namna gani wapo tayari kuchangia maendeleo ya elimu nchini na kwamba kiasi cha fedha ambacho kitachangiwa kitabaki ndani ya Mkoa kwa ajili ya maendeleo ya elimu.

Akitoa mada ya Mfuko wa kusaidia maendeleo ya elimu Duniani (GPE) kwenye kikao hicho,Mwezeshaji Mathias Tilia amevitaja vigezo vinavyotumika ili nchi iweze kupata ufadhili kupitia mfumo wa MG kuwa ni kila Dola tatu za Marekani zitakazotolewa na wadau wa maendeleo wa nje,GPE itatoa Dola moja ya Marekani.

Ameongeza kuwa kila Dola moja ya Marekani itakayotolewa na wadau wa maendeleo ya elimu nchini,GPE itaoa Dola moja ya Marekani.

 Amesema Wizara ya elimu imekusudia kuandaa hafla ya kuhamasisha wadau wa elimu nchini ili waweze kufadhili na kuongeza ufadhili kwenye masuala ya elimu msingi na kwamba fedha hizo zitachangia kuiwezesha serikali kutekeleza mipango mipya iliyoibuliwa sanjari na mabadiliko ya Sera na mitaala ya elimu ili kutekeleza eneo la mafunzo ya amali

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.