• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFANYAKAZI wa Ruvuma waiomba Serikali kutatua changamoto za kitumishi kwa wakati

Imewekwa kuanzia tarehe: May 2nd, 2022

WAFANYAKAZI wa Mkoa wa Ruvuma wameiomba Serikali kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu changamoto zao za kiutumishi.

Ombi hilo llimetolewa katika risala ya watumishi hao iliyosomwa na Mratibu wa Chama cha TUCTA Ashirafu Chussi katika maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika kimkoa Wilaya ya Namtumbo.

Risala hiyo imezitaja baadhi ya changamoto zinazowakabili watumishi kuwa ni mishahara ya watumishi bado ni midogo ukilinganisha na gharama za maisha hivyo wameiomba Serikali kuongeza mishahara na kuboresha maslai ya watumishi.

‘’Tunaiomba Serikali kupitia Mei Mosi hii kwa jicho la pekee kabisa iongoze mishahara na kuboresha maslahi kwa wafanyakazi kwa muda mrefu  mishahara haijaongozwa takribani miaka sita sasa’’, imeeleza risala hiyo.

Watumishi hao wamesema kutoongeza mishahara kwa muda mrefu kunashusha morali ya utendaji kazi kwa wafanyakazi na kusababisha kutoa huduma duni kwa jamii.

Kulingana na risala hiyo changamoto nyingine zinazowakabili watumishi wa Mkoa wa Ruvuma ni baadhi ya watumishi kutolipwa madeni kwa wakati na baadhi ya waajiri kutolipa nauli za watumishi na mizigo yao pindi wanapostaafu.

Changamoto nyingine wamezitaja kuwa ni baadhi ya waajiri  kuendelea kufanya kikao kimoja tu cha Baraza la wafanyakazi ili kupitisha bajeti na wengi wao kutolipa stahiki sahihi za wajumbe kwa mujibu wa muongozo kwa mfano 2022 kati ya Halmashauri nane za Mkoa wa Ruvuma ni Halmashauri moja tu ya Manispaa ndio imelipa.

Kwa mujibu wa risala hiyo baadhi ya waajiri kutopeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa wakati na kusababisha baadhi ya watumishi kutolipwa stahiki zao za mafao kwa wakati na baadhi ya watumishi kufanyishwa kazi siku za mapumziko bila kulipwa stahiki zao za saa za ziada.

Hata hivyo uwepo muongozo mpya kandamizi wa upandishaji wa madaraja ya mishahara unaotaka mtumishi wa ajira mpya kukaa miaka mitano na miaka minne kwa aliyopo kazini ili kupata sifa ya kupandishwa daraja ni changamoto kubwa kwa wafanyakazi wetu.

Licha ya changamoto hizo wafanyakazi wa Mkoa wa Ruvuma wameahidi  kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa maslahi mapana ya Nchi yetu na Mkoa huku wakiamini Serikali itachukua hatua kwa wakati kutatua changamoto hizo.

Akijibu risala hiyo mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Dkt Julius Ningu ameahidi Serikali kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu changamoto hizo.

Hata hivyo RC Ibuge ametoa rai kwa waajiri kuhakikisha wanajitahidi kuzingatia maslahi kwa watumishi na kulipa madeni kwa wakati sanjari na kuandaa nauli za watumishi na mizigo yao kuandaliwa kwa wakati.

‘’Natoa maelekeza kwa waajiri wote kuhakikisha wanazingatia muongozo uliowekwa na Serikali katika kushughulikia stahiki za watumishi na kupeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii’’, amesema RC Ibuge.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Mei Mosi 2022 ni mishahara na maslaHi bora kwa wafanyakazi ndio kilio chetu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Mei 2,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.