• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFUGAJI Tunduru kuanza kupewa elimu ya kifua kikuu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 14th, 2023

HOSPITALI ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma kupitia kitengo cha kifua kikuu na ukoma kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo shirika lisilo la kiserikali la MDH,imeanza kutoa elimu na upimaji wa ugonjwa wa kifua kikuu kwa jamii ya wafugaji katika maeneo wanayoishi.

Hatua hiyo inatokana na kundi hilo kubwa, kuwa miongoni mwa makundi yaliyopo hatarini kupata maambukizi ya ugonjwa huo unaotajwa  kupoteza maisha ya watu wengi Duniani hasa katika nchi za kusini mwa Bara la Afrika.

Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa wilaya ya Tunduru Dkt Mkasange Kihongole alisema,jamii ya wafugaji iko kwenye hatari ya kupata ugonjwa huo kutokana na maisha wanayoishi hasa unywaji wa maziwa ya ng’ombe yasiyochenshwa vizuri.

Alisema,unywaji wa maziwa ya ng’ombe holela  ni hatari kwani yana vimelea ambavyo ni chanzo kikubwa cha kuenea kwa ugonjwa wa kifua kikuu na kuitaka jamii kuepuka kunywa maziwa yasiyochemshwa,badala yake  watumie maziwa yaliyochemshwa ambayo ni salama na hayana madhara kwa binadamu.

Alisema,wilaya ya Tunduru inatajwa kuwa miongoni mwa wilaya zenye maambukizi makubwa ya  kifua kikuu hapa nchini,na sababu mojawapo ya kuongeza kwa ugonjwa huo ni unywaji holela wa maziwa ya ng’ombe wasiopimwa afya zao.

Kihongole alitaja makundi yaliyo katika hatari ya kupata maradhi hayo ni wazee,kwani binadamu  kadri  umri unavyokuwa mkubwa kinga za mwili zinapungua na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.

Kwa mujibu wa Kihongole,makundi mengine ni wasafiri,watu wanaoishi katika msongamano wakiwemo wafungwa,wanafunzi na wanaoishi kwenye nyumba ambazo hazina hewa au mwanga wa kutosha.

Ametaja dalili za mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo ni kukohoa kwa wiki mbili au zaidi,kutokwa na jasho jingi hasa nyakati za usiku,kupungua uzito,kupoteza hamu ya kula na kwa watoto kulia lia, kuwa na homa za mara  kwa mara na kuchelewa kukua.

Kwa upande wake Afisa mipango wa shirika la MDH mkoani Ruvuma Dkt Hellen Mwita,ameikumbusha jamii kuwa na utaratibu wa kwenda katika vituo vya kutolea huduma kwa ajili ya uchunguzi wa afya za  mara kwa mara.

Dr Mwita ametoa wito kwa akina mama,pindi wanapoona dalili za ujauzito ni vema kwenda kliniki mapema ili kupata ushauri wa wataalam na wanatumia zahanati na vituo vya afya vilivyopo kujifungulia,badala ya kubaki nyumbani kwani ni hatari kwa afya zao na watoto wakati wa kujifungua.

Diwani wa kata ya Misechela Zuberi Diwani,amewataka wafugaji kubadilika na kuanza kushiriki  katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kuhudhuria  kampeni  za uchunguzi  wa afya zinazoendeshwa na wataalam wa wizara ya afya na wadau wengine.

Ameishukuru serikali kupitia Hospitali ya  wilaya ya Tunduru kitengo cha kifua kikuu na ukoma,kwenda kufanya uchunguzi wa ugonjwa wa kifua kikuu kwa jamii ya wafugaji ambayo kwa muda mrefu haiwajawahi kufikiwa na huduma zozote za afya kwenye maeneo yao.

Laisi Maduka mfugaji,ameiomba serikali  kupeleka huduma hizo mara kwa mara kwenye maeneo yao ili waweze kupata matibabu,kwa kuwa wengi wao wanaishi mbali na maeneo ya kutolea huduma za afya.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.