• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKANDARASI wazawa Ruvuma wampa kongole Rais Samia

Imewekwa kuanzia tarehe: March 13th, 2023

WAKANDARASI wazawa wanaotekeleza miradi ya ujenzi wa barabara mkoani Ruvuma, wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na serikali yake ya awamu ya sita kwa kuwaamini na kuwapatia miradi mingi  iliyowajengea uwezo zaidi na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa.

Aidha,wamempongeza Rais Samia kuipatia fedha za kutosha,wakala wa barabara za vijijini na mijini(Tarura) zilizowezesha wakandarasi wazawa kupata kazi,hali ambayo imewasaidia  kupata kipato cha kuhudumia familia na kuchangia maendeleo ya mkoa huo.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Valence Urio amesema,katika kipindi cha miaka miwili cha Rais Dkt Samia kumekuwa na mafanikio makubwa kwani miradi mingi ya barabara za vijijini na mijini zimetekelezwa na wakandarasi wazawa.

Urio ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Ovans Construction Ltd amesema,kabla ya serikali ya awamu ya sita kuingia madarakani changamoto kubwa ilikuwa miradi  mingi inayotangazwa,michache ndiyo iliyotekelezwa tofauti na  awamu ya sita ambapo miradi inayotangwa inatekelezwa na wanapewa wakandarasi wa ndani(wazawa).

Amesema kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa na serikali kwenye sekta ya Barabara, imewafanya wakandarasi kutosheka na kubaki katika mkoa mmoja au miwili tu, badala ya kuzurura kwenda mikoa mingine kutafuta kazi.

“Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuturejeshea fursa hii ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati,miaka ya nyuma tumepitia wakati mgumu kwani kazi nyingi za ujenzi wa miradi ya barabara walipewa wakandarasi wakubwa hasa kutoka nje.”alisema Urio.

Pia amefurahishwa na uamuzi wa Rais Dkt Samia,kuwapunguzia tozo ikiwemo kulipia galantii kwenye miradi yote,lakini kutokana na maboresho ya sheria iliyofanywa na serikali ya awamu ya sita kuondoa utaratibu huo  sasa mkandarasi analipia shilingi bilioni moja tu kwenye kazi zote.



Urio,ameiomba serikali kuendelea kuwaamini  wakandarasi wa ndani na kuwapa kazi za ujenzi wa miradi mikubwa ya maendeleo kwani sasa wana uzoefu wa kutosha na uwezo mkubwa.

Amewaasa wakandarasi wenzake kubadilika,kufanya kazi kwa weledi,uaminifu na kufanya kazi zenye ubora ili kurudisha imani kwa serikali na waweze kushindana na wakandarasi wa nje.

Kwa upande wake Meneja wa TARURA wilayani Mbinga Oscar Mussa amesema,katika miaka miwili ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita wamefanikiwa kufungua barabara mpya zenye urefu wa kilomita 500,kujenga madaraja na makalavati 106 na kujenga  barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 5.67.

Ameishukuru Serikali kuiongezea fedha Tarura wilaya ya Mbinga ambapo mwaka wa fedha 2021/2022 walipokea  jumla ya shilingi bilioni 4.5 ambazo  zimewezesha kufanya matengeneza barabara  zenye urefu kilomita 287.77 kujenga barabara kwa kiwango cha  lami urefu wa kilomita 2.17 na kujenga madaraja makubwa na madogo 53.

Amesema,kwa mwaka wa fedha 2022/2023 wametengewa shilingi bilioni 5.8 kutoka bilioni 4.5 za mwaka  uliopita,na fedha hizo zimetumika kujenga barabara kwa kiwango cha lami kilomita 3.5,kufungua na kufanya matengenezo ya barabara kilomita 217,kujenga madaraja makubwa na madogo na makalavati 53 na kufunga taa za barabarani 30 katika wilaya yote ya Mbinga.

Amewataka wananchi na watumiaji wa barabara hizo,kujiepusha na uharibifu wa miundombinu ya barabara kwa kutozidisha uzito wa magari,kufanya shughuli za kibinadamu kando kando ya barabara na kuacha kupitisha mitaro ya maji ili barabara hizo ziweze kudumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.