• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKAZI wa Madaba waanza kunufaika na mradi wa maji wa bilioni 1.3

Imewekwa kuanzia tarehe: January 18th, 2021

MRADI wa maji unaotekelezwa katika vijiji vinne vya Mtepa,Kipingo,LItuta na Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 na tayari wananchi wa kijiji cha Kipingo wameanza kupata maji.

Meneja wa Mamlaka ya Maji vijijini RUWASA Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles amesema mradi huo umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.3  ambapo matanki mawili yamejengwa,huku tanki moja la Kipingo limejazwa maji kwa ajili ya kuanza kuhudumia wananchi.

Hata hivyo amesema ili kukamilisha tanki moja la Madaba pachani zinasubiriwa pampu za kusukumia maji ambazo zitafungwa wakati wowote kuanzia sasa na kwamba mradi huo ni mkubwa  umehusisha ujenzi wa matanki mawili na ulazaji wa mabomba kilometa 34.

“Wananchi wa kipingo wameanza kupata maji,tunatarajia maeneo mengine yaliyobakia kati ya Januari 18 hadi 25 mwaka huu,wananchi wataanza kupata huduma ya maji,tunamshukuru mheshimiwa Rais kwa kutupatia fedha zilizotekeleza mradi huu hivyo kuondoa kero ya maji kwa wananchi’’,alisema Charles.

Olaph Pilli ni Diwani wa Kata ya Lituta Halmashauri ya Madaba,amesema kabla ya kutekeleza mradi huu,Madaba ilikuwa na changamoto kubwa ya maji ambapo amesema mradi huu wa maji umekuwa mkombozi mkubwa katika kata yake.

“Hali ya maji katika Halmashauri yetu ya Madaba hasa katika Kata ya Lituta ilikuwa ni tete,wananchi walikuwa wanapata shida ya maji,lakini baada ya mradi huu sasa Madaba haitakuwa na shida tena ya maji,tuna maji ya kutosha’’,alisisitiza Diwani Pilli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumiaji maji vijiji vinne vya Mtepa,Kipingo,Lituta na Madaba Modestus Mgina ameipongeza RUWASA kwa kukamilisha ujenzi wa mradi huo ambapo tayari tanki moja la Kipingo limejazwa maji tayari kwa kuanza kusambazwa kwa wananchi.

Amesema mradi huo unakwenda kuwanufaisha wananchi zaidi ya 19,000 ambapo ameitaja hali ya maji kabla ya kutekeleza mradi huu ilikuwa ni mbaya,wananchi walikuwa wanapata maji ya mgawo kati ya siku tatu hadi tano.

“Maji yalikuwa yanapatikana kwa vurugu na ugomvi mkubwa,ilikuwa ni vita ya maji,lakini sasa mradi huu unamaliza kero hiyo,tunamshukuru sana Rais Dkt.John Magufuli,tuna raha sana kupata mradi huu’’,,alisema.

Desderia Ngatunga ni Mkazi wa Madaba akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Madaba, amesema wanaishukuru serikali kwa kuwapatia mradi mkubwa wa maji ambapo sasa Madaba itaneemeka kwa maji mengi ya kutosha na kumaliza kilio cha maji cha miaka mingi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 18,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.