• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANAFUNZI Mbinga waishukuru serikali kwa madarasa na samani

Imewekwa kuanzia tarehe: May 12th, 2023

WANAFUNZI wa shule ya Sekondari Makita Halmashauri ya Mji Mbinga mkoani Ruvuma,wameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea vyumba viwili vya madarasa.

Wakizungumza  kwa nyakati tofauti  walisema,mradi huo wa umewaondolea adha ya kubanana katika kichumba kimoja na vitawapa fursa ya kukaa kwa nafasi na kuwaongezea morali ya kusoma kwa bidii.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake John Kapinga alieleza kuwa,ujenzi wa madarasa hayo yatakuwa chachu katika safari yao ya masomo, kwa kuwa walimu nao watapata nafasi kubwa ya kuwafundisha na wao kuwaongezea umaskini wa kusikiliza wanachofundishwa darasani.

Mkuu wa shule hiyo Emmanuel Mwamasika alisema,shule hiyo ilipokea kiasi cha Sh.milioni 40 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa.

Alisema,kati ya fedha hizo Sh.milioni 31,493,400.00 zimetumika kununua vifaa vya ujenzi,Sh.milioni 5,841,600.00 zimetumika kulipa gharama ya ufundi na Sh.milioni 2,665,000.00 kutengeneza viti na meza 41.

Mwamasika alieleza kuwa,Halmashauri ya Mji Mbinga imechangia jumla ya Sh.milioni 2,535,000.00 kwa ajili ya kuongeza viti na meza 39 na wananchi wamechangia nguvu kazi kwa kuleta kokoto zinazokadiriwa kuwa na gharama ya Sh.600,000.

Mwamasika alisema, baada ya kukamilika mradi huo umesaidia kuondoa uhaba wa vyumba vya madarasa na kupunguza msongamano kwa wanafunzi darasani,wanafunzi kukaa katika mazingira mazuri ya kujifunzia na kufundishia na kuinua taaluma kwa kuwa wanafunzi watasoma katika mazingira mazuri.

Aidha alisema,vyumba hivyo vitatoa fursa kwa wanafunzi kupata elimu itakayowasaidia katika mapambano dhidi ya Rushwa,maralia,lishe duni,kuimarisha usawa na hata kutokomeza ukatili wa kijinsia na unyanyapaa.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 Abdalla Shaibu Kaim,ameipongeza Halmashauri ya mji Mbinga kwa usimamizi wa mradi huo ambao umewasaidia sana wanafunzi kuondokana na changamoto ya kukaa  wengi katika chumba kimoja.

Amewaasa watumiaji wa majengo hayo wanafunzi na walimu,kuhakikisha wanatunza majengo hayo ili yaweze kuwasaidia kupata elimu bora ambayo itawasaidia kupambana na changamoto mbalimbali na kutimiza malengo yao.

Amemtaka Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauari hiyo kuhakikisha anatumia weledi katika majukumu yake na kutanguliza uzalendo mbele, badala ya kufanya kazi kwa kulipua kwa sababu serikali inaingia gharama kubwa katika kutekeleza miradi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.