• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI 11,080 wa Kata za Ngumbo na Liwundi kunufaika na maji ya RUWASA

Imewekwa kuanzia tarehe: March 22nd, 2025

Wakazi  wapatao 11,080 kutoka vijiji vya Ngumbo, Mbuli, Mkili, Liwundi na Yola wilayani  Nyasa mkoani Ruvuma wanatarajiwa kupata huduma ya maji safi na salama kupitia mradi wa maji wa Ngumbo Group awamu ya pili.

Hatua hii itawezesha wananchi kutumia muda mwingi kwenye shughuli za kiuchumi na kupunguza magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Nyasa, Mhandisi Evath Rwekaza, amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 75.

“Tayari baadhi ya wananchi wameanza kupata huduma kupitia vituo vya maji vilivyojengwa na maunganisho binafsi”,alisema Rwekaza.

Naye Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Martin Manyanya, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo, amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi bila kujali hali zao za kiuchumi.

Amesisitiza kuwa serikali inajitahidi kuhakikisha kila mwananchi anapata maji safi na salama kwa maendeleo ya jamii.

Kwa upande wao Madiwani wa kata za Ngumbo na Liwundi wameeleza furaha yao kwa serikali baada ya miradi ya maji kufanikisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Mradi wa Maji wa Ngumbo Group awamu ya pili unatekelezwa na Mkandarasi Mzawa, NIPO AFRICA ENGINEERING COMPANY LIMITED kutoka Dodoma, kwa gharama ya zaidi ya Shilingi bilioni 2.

Mradi huu unafadhiliwa na Mfuko wa Maji wa Taifa (NWF), Serikali Kuu (GoT), na P4R. Utekelezaji ulianza Novemba Mosi 2023, na awali ulitarajiwa kukamilika Aprili 30, 2024, lakini kutokana na changamoto mbalimbali, muda wa utekelezaji umeongezwa hadi Juni 30, 2025.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.