• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Songea waiomba TARURA kufanya matengenezo barabara zilizoharibika

Imewekwa kuanzia tarehe: April 11th, 2024

WAKAZI wa mitaa mitatu ya Osterbay,Miembeni na Kiswele kata ya Msamala Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma,wameiomba serikali kupitia wakala wa barabara za mijini na vijijini(TARURA)kufanya matengenezo ya barabara zake ili ziweze kupitika kirahisi.


Wamesema,kwa sasa barabara nyingi kwenye maeneo hayo ni mbovu na baadhi ya watu wanalazimika kulipia gharama ya kupaki magari yao kwenye vituo vya mafuta kwa kuwa wanashindwa kufika nayo nyumbani.


Menald Mwanditi mkazi wa mtaa wa Kiswele asema,katika kipmeindi hiki ambacho mvua bado zinaendelea kunyesha kwa wingi, hali inakuwa mbaya zaidi hasa maji yanayotoka barabara kuu ya Songea-Makambako iliyoko chini ya wakala wa barabara Tanzania (TANROADS).


Amesema,katika barabara hiyo kuanzia katikakituo cha mafuta Ottawa hadi Chuo cha Top One Inn maji yanapita juu ya barabara na kuelekea upande wa pili ambako kuna makazi ya watu kwa kuwa yanashindwa kupitia kwenye mifereji ambayo imeziba kutokana na kujaa mchanga na takataka mbalimbali.


Kwa mujibu wa Mwanditi,barabara nyingi za mitaa za TARURA kwa sasa zimeharibika na hazipitiki kwa kuwa hazijafanyiwa ukarabati wowote tangu zilipotengenezwa hivyo kuwa na mashimo makubwa yanayojaa maji na kuhatarisha usalama hasa kwa watoto wadogo.

Mkazi wa Msamala Leonald Kapinga amesema, kukosekana kwa mifereji ya kupitisha maji ya mvua katika barabara kuu ya Songea-Makambako ina sababisha mchanga unaosombwa na maji kujaa kwenye makazi yao na hivyo kuingia gharama kubwa ya kuondoa mchanga huo.

Ameiomba TARURA na TANROADS mkoani Ruvuma,kufanya matengenezo ya barabara zao ili kuwaondolea adha inayowakabili kwani kuna hatari ya kufunga biashara zao kwa kukosa wateja.
Kaimu Meneja wa TARURA wilaya ya Songea Godfey Mngale amesema,kabla ya kilio cha wananchi wa Msamala,tayari serikali kupitia TARURA ilishaanza kuchukua hatua kwa kufanya matengenezo ya barabara katika mitaa hiyo.


Amesema,tatizo lililojitokeza kwa sasa ni Mkandarasi amelazimika kusimamisha kazi kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha,lakini mara mvua zitakapokatika kazi ya matengenezo ya barabara katika maeneo hayo zitaendelea kama kawaida.
Amewatoa hofu wananchi wa Msamala kuhusu ubovu wa barabara na kusisitiza kuwa,serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imejipanga kwa kuhakikisha inaboresha miundombinu ya barabara zote ili kurahisisha usafiri na usafirishaji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.