Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Komred Oddo Mwisho, amewataka wanawake na vijana, kujitokeza kwa wingi kushiriki katika siasa na nafasi za uongozi ili kuchangia maendeleo ya taifa.
Mwisho alitoa wito huo akiwa mgeni rasmi katika matembezi ya hisani ya Wanalizombe Marathon yaliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na Fro Events.
Matembezi hayo yaliyobeba ujumbe wa “Umoja, Amani, Ushiriki wa Vijana na Wanawake katika Uongozi wa Kijamii kwa Demokrasia,” yalihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa serikali na chama,
Mwisho aliwapongeza waandaaji na washiriki kwa kujitokeza kwa wingi, akisisitiza kuwa tukio hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha uchaguzi wa amani na ushiriki wa wananchi katika uongozi.
Alibainisha zaidi kuwa wanawake wa Mkoa wa Ruvuma wanapaswa kutumia haki yao ya kikatiba kugombea nafasi za uongozi kwa kuwa wao ni msingi wa jamii na maendeleo ya taifa.
Aidha, alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi wake thabiti unaoendelea kuboresha maisha ya wananchi kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.