• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATANZANIA washauriwa kuendeleza urithi wa utamaduni wa Mtanzania

Imewekwa kuanzia tarehe: February 23rd, 2024

Mkuu  wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewashauri watanzania kuenzi,kutunza na kuendeleza urithi wa utamaduni wa asili kwa ajili ya manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kanali Thomas ametoa ushauri huo wakati anafungua Tamasha la miaka 119  ya kumbukizi ya mashujaa wa vita ya Majimaji na utalii wa utamaduni  kwenye viwanja ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.

Ameutaja urithi wa utamaduni kuwa ni tunu na kioo cha Taifa la Tanzania na kwamba unaleta umoja,amani na mshikamano wa kitaifa  ikiwa ni Pamoja na kulitambulisha Taifa la Tanzania Duniani.

“Natoa rai kuendelea kuibua na kuendeleza fursa za utalii wa utamaduni zinazopatikana katika Mkoa wa Ruvuma na Ukanda wa Kusini kwa ujumla ili kuinua Uchumi na kuboresha hali ya Maisha ya wananchi wa eneo hili’’,alisisitiza RC Thomas.

RC Thomas ameutaja Mkoa wa Ruvuma kuwa ni miongoni mwa mikoa michache nchini ambao umejaliwa  kuwa na ardhi yenye rutuba,madini,mito hifadhi za  wanayamapori na vivutio vingine vinavyoweza kuchochea maendeleo ili kuuvusha Mkoa kutoka sehemu moja na Kwenda sehemu nyingine.

Akizungumzia tamasha hilo,Mkuu wa Mkoa amesema kila mwaka kuanzia Februari 23 hadi 27 linafanyika tamasha la kumbukizi ya mashujaa wa vita ya Majimaji wakikumbukwa mashujaa 67  walionyongwa mjini Songea na  wajerumani   Februari 27,1906 ,wakitetea maslahi ya nchi ya Tanganyika.

Kwa upande wake Kaimu Mhifadhi wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Rozi Kangu akitoa taarifa ya makumbusho ya kumbukumbu ya vita ya Majimaji,amesema historia hiyo inaanzia mwaka 1905 hadi 1907 baada ya mashujaa 67 kukamatwa na kunyongwa kikatili na wajerumani kisha kuzikwa kwenye makaburi mawili yaliyopo ndani ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji.

Amesema makumbusho ya Majimaji yalianzishwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Hayati Dkt.Lawrence Gama mwaka 1980 na mwaka 2009 makumbusho hayo yalikabidhiwa kwa Shirika la Makumbusho ya Taifa kwa mujibu wa sheria ya makumbusho ya Taifa namba 7 ya mwaka 1980.

Amesema kilele cha maadhimisho hayo ni Februari 27,2024 ambapo Februari 24,2024 yatafanyika mashindano ya ngoma za asili  kutoka Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma na Februari 25,2024 litafanyika kongamano la kurithisha urithi wa utamaduni mjini Mbambabay wilayani Nyasa.

Naye Chifu wa Tano wa Kabila la Wangoni Nduna Emanuel Zulu Gama amesema katika maadhimisho ya mwaka huu amewaalika machifu kutoka nchini Malawi na mikoa mingine ambayo ni Njombe,Iringa,Tabora,Mwanza,Lindi na Mtwara.

Kaulimbinu ya kumbukizi ya mashujaa wa  vita ya Majimaji mwaka huu ni Majimaji ni ukombozi wa Bara la Afrika na matumizi ya rasilimali zake ni urithi wetu kwa maendeleo ya utalii na Uchumi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.