• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZAZI wanaolazimisha watoto wao kufeli kuwajibishwa

Imewekwa kuanzia tarehe: April 29th, 2021

Wazazi na walezi Wilayani Mbinga wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kukua kwa elimu na wale wote watakaobainika kuhujumu jitihada za serikali katika kukuza sekta ya elimu kwa kuhamasisha watoto wao kufanya vibaya kwa makusudi kwenye mitihani yao wamepewa onyo kali na kwamba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Tathmini ya Elimu Tarafa ya Mbuji kilichofanyika Aprili 22, ambapo baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho wameibua hoja na mjadala kuhusu baadhi ya wazazi na walezi kuhujumu kwa makusudi jitihada za serikali katika kuboresha elimu kwa namna mbalimbali na kupelekea watoto kufanya vibaya kwenye mitihani yao ya mwisho licha ya wanafunzi hao kuwa na uwezo mzuri darasani.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Mtakatifu Charles Borromeo, Kijiji cha Myau kata ya Mbuji na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu, Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma, Emmanuel Kisongo amesema suala la usimamizi na ukuaji wa sekta ya elimu ni wajibu wa kila mmoja katika jamii nzima kuanzia ngazi ya familia na kwamba ni aibu kubwa kwa mzazi kulazimisha na kusababisha mtoto wake kufeli mtihani.

Bw. Kisongo amesisitiza kuwa jukumu la usimamizi wa elimu ni la kila mmoja na kwamba changamoto nyingi zilizotolewa kwenye kikao hicho zipo ndani ya uwezo wa jamii akitolea mfano utoro, mimba kwa wanafunzi, wazazi kutochangia chakula na mahitaji muhimu huku akitoa wito kwa jamii kuacha kulalamika na kutaka kila mmoja kekemea, kuchukua hatua na kuwajibika kulingana na nafasi yake.

“Wajibu wa usimamizi wa elimu ni wetu sote, hakuna kulalamika tuchape kazi na kukemea maovu hakuna mtu wa kukomboa watoto na jamii ya mbinga zaidi ya sisi wenyewe; tukiamua tunaweza” Amesema Bw. Kisongo. 

Imeelezwa kuwa baadhi ya wazazi wamekua wakiwapa vitisho watoto wao kwa kuwalazimisha kutoandika majibu sahihi kwenye mitihani, kuwatorosha watoto kipindi cha mitihani, kukwepa kutoa michango na mahitaji ya shule huku baadhi wakidaiwa kujihusisha na imani za kishirikina mashuleni na kupelekea wanafunzi kwenye shule hizo kushuka kitaaluma.

Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwl. Samwel Komba ambaye ni Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ametoa taarifa kuwa hadi sasa jumla ya wanafunzi wanne (4) wamepata mimba, watatu kati yao wakiwa tayari wameshaandikishwa kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu na kukemea tabia ya baadhi ya wazazi na jamii kukwepa kutoa ushahidi na kesi nyingi kumalizwa nje ya mahakama na kuwataka kutoa ushirikiano kila wanapotakiwa kufanya hivyo.

Kikao cha Tathmini ya Elimu Tarafa ya Mbuji kimefanyika ikiwa ni mwendelezo wa vikao hivyo vinavyofanyika kwenye ngazi ya Tarafa ili kufanya tathmini ya hali ya ukuaji wa taaluma kwa kubainisha, kupitia na kujadili changamoto mbambali zinazoikabili sekta ya elimu na kuweka mikakati na maazimio ya pamoja yanayokusudia kuinua hali ya taaluma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kushirikisha wadau wa elimu kama Madiwani, Watendaji wa Kata na Vijiji, Maafisa Elimu na wataalamu wengine ngazi ya kata na vijiji, wajumbe wa bodi na Kamati za Shule na wadau wengine muhimu.


Imeandikwa na: Salum Said

Afisa Habari Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.