• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZAZI watahadharisha,asilimia 67 ya watoto hutumia mitandao bila uangalizi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 16th, 2023

WAZAZI  wametahadharishwa kuzingatia usalama wa mtoto katika ulimwengu wa kidijitali kutokana na takwimu hapa nchini kuonesha kuwa asilimia 67 ya Watoto wenye umri kuanzia miaka 12 hadi 17 wanatumia mitandao bila usimamizi.

Tahadhari hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Kapenjama Ndile katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika,kimkoa yamefanyika katika uwanja wa Rwinga mjini Namtumbo.

Kanali Thomas amesema takwimu zinaonesha kuwa katika kila nchi  duniani,Watoto ndiyo kundi linaloongoza kwa utumiaji wa bidhaa  za mawasiliano bila kuzingatia matumizi sahihi.

Amebainisha zaidi kuwa  Watoto wengi wanatumia mitandao mbalimbali ikiwemo simu za ndugu zao,walezi,wazazi na marafiki hivyo ametoa rai kwa jamii kuhakikisha Watoto wanaelekezwa kuzingatia matumizi sahihi na salama dhidi ya vifaa vya kieletroniki kutokana na kasi ya uwepo wa vitendo vya ukatili vinavyofanyika mtandaoni.

Ametoa rai kwa kila mzazi na mlezi kuhakikisha mtoto hatumii vifaa vya kieletroniki kama simu,intaneti na luninga bila uangalizi wa karibu ili kumepusha kujiingiza kwenye maeneo hatarishi ya kufanyiwa ukatili wa mtandaoni.

“Mkoa wa Ruvuma na mikoa mingine nchini,bado tunakabiliwa na vitendo vya ukatili wa aina mbalimbali ikiwemo ubakaji,ulawiti,utumikishaji katika ajira hatarishi,ndoa na mimba za utotoni’’,alisisitiza.

Hata hivyo Kanali Thomas,amekemea tabia ya baadhi ya wanaume kurithi wajane na kutelekeza Watoto kwa kuwaacha wanaangaika bila huduma za msingi ambapo amesema vitendo hivyo vimekithiri na kuendelea kuripotiwa katika vituo vya polisi,ustawi wa jamii na katika ngazi zote za kaya,Kijiji,kata,wilaya hadi mkoa.

Ametoa rai kwa viongozi wote wa serikali na madhehebu ya dini kuwajibika kwa kuwalinda Watoto na kuwapeleka shule,kuwalea na kuwapa haki zao za msingi kama chakula,matibabu.malezi bora na kuwalinda dhidi ya unyanyasaji.

Amesema Mkoa wa Ruvuma unaendelea kutoa huduma mbalimbali kwa watoto ikiwemo elimu kwa Watoto kuanzia shule za awali,msingi,sekondari hadi vyuo vikuu na kutoa huduma ya afya zikiwemo chanjo kwa Watoto ili  kuepuka maradhi na kuwa na afya bora.

Awali akisoma risala ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika,mwanafunzi wa shule ya msingi Namtumbo Amina Said   alisema maadhimisho hayo yanafanyika kila mwaka Juni 16,kuendeleza kumbukumbu ya mauaji ya Watoto zaidi ya 600  yaliyofanywa na makaburu katika kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya kusini Juni 16,1976.

Watoto hao wa kiafrika waliuawa baada ya kuandamana ili kudai haki zao za msingi kama vile kutobaguliwa katika mfumo wa kupata elimu,afya na kunyanyaswa na makaburu.

Hata hivyo katika risala hiyo Watoto hao wameishukuru serikali ya Awamu ya Sita kwa kiwango kikubwa kuwapatia Watoto wa Tanzania fursa sawa katika masuala mbalimbali yakiwemo elimu,afya na ulinzi kuanzia ngazi ya familia,wilaya hadi mkoa

Kauli mbiu ya maadhimisho ya maadhimisho ya siku yam toto wa Afrika 2023 ni zingatia usalama wa mtoto katika ulimwengu wa kidijitali.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.