• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI Jenista ahimiza kutangaza vivutio vya utalii wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: August 18th, 2022

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi  wa umma na utawala Bora Jenista Mhagama,amezindua rasmi Hoteli ya kisasa ya CANOPIES iliyopo mtaa wa Making’inda Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Waziri Mhagama,amewaomba wafanyabiashara wa ndani na nje kuja kuwekeza zaidi mkoani Ruvuma kwenye sekta ya utalii na Hoteli kwani mkoa huo ni eneo bora na salama kwa ajili ya kuwekeza kutokana na kuwa na vivutio vingi vya utalii ikilinganisha na maeneo mengine hapa nchini.

Alisema,serikali ya awamu ya sita itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji huku akiwataka wakazi wa mkoa wa Ruvuma hususani vijana kujifunza kwa vijana kutoka mikoa mingine  walioamua kuwekeza miradi ya maendeleo mkoani Ruvuma badala ya kukimbilia kwenda maeneo mengine.

Alisema,mkoa wa Ruvuma bado kuna fursa  kubwa ambayo zinahitaji kuwekezwa hasa kwenye miradi mbalimbali itakawezesha kubadilisha taswira ya mkoa huo unaotajwa kuwa na vivutio mbalimbali vya utalii ikiwamo ziwa nyasa,hifadhi ya Taifa ya Nyerere na meoneo mengine yanye utajiri ambayo bado hajafanyiwa kazi.

“kuna tatizo kubwa la ajira katika mkoa huo wetu,kwa hiyo tukifungua miradi kama hii itawezesha kusaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wetu wa mkoa wa Ruvuma na kupanua wigo wa ulipaji kodi kwa serikali”alisema Mhagama.

Alisema,uwekezaji huu wa Hoteli ya Canopies unakwenda kufungua shughuli za kiuchumi katika manispaa ya Songea na mkoa wa Ruvuma na kuwataka viongozi wa mkoa wa Ruvuma kuwatambua,kuwasaidia  na kuwaunganisha vijana wa mkoa huo na taasisi za fedha  zinazoweza kutoa mikopo rahisi na yenye riba nafuu.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa huo Kanali Laban Thomas alisema,ufunguzi wa Hoteli ya Canopies ni mafanikio ya mwaka mmoja wa uongozi wa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Suluhu Hassan.

Amempongeza Mkurugenzi wa Hoteli hiyo Desdery Rutta, kwa uthubutu wake wa kujenga Hoteli ya kisasa ambayo inakwenda kuongeza idadi ya nyumba za kulala wageni katika mkoa wa Ruvuma na kutoa wito kwa vijana wengine kuiga mfano huo.

Alisema,ujenzi wa Hoteli hiyo mbali na kutoa ajira kwa vijana wa mkoa wa Ruvuma pia itaongeza wigo wa usimamizi wa mapato na ukusanyaji wa kodi za serikali  ili kwenda sambamba na malengo ya serikali yetu.

Akizungumzia juu ya ujenzi wa barabara ya lami kutoka eneo la Ottawa hadi Hotelini hapo Mkuu wa mkoa alisema, tayari serikali iko katika hatua ya mwisho ya kujenga barabara ya lami kutoka Seed farm hadi uwanja wa ndege km 26 ambayo itapita kando kando ya Hoteli hiyo.

Awali Mwakilishi wa Hoteli hiyo Veronica Gondwe alisema, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa sekta ya utalii jambo ambalo limekuja wakati muafaka kwao.

Alisema,ujenzi wa Hoteli ya Canopies ulianza rasmi mwaka 2014 ikiwa ni katika juhudi za uwekezaji wa ndani na nje kwa kuzingatia kuwa  imejengwa karibu na mlima Chandamali ambao una vivutio vya aina yake kama  vile pango la kale,miti ya asili na nyuki wapole wasiouma hasa ukiwa ndani ya pango hilo.

Alisema,Hoteli hiyo ina vyumba 16 vya kulala na vyenye hadhi ya madaraja tofauti kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya wageni watakaokwenda  na imesaidia sana kutengeneza ajira kwa vijana wa mkoa wa Ruvuma na kufungua fursa na soko la bidhaa mbalimbali kwa wananchi wanaozunguka  eneo hilo kwa kuuza mboga mboga,mayai,kuku na matunda.

Aidha alisema,mpango wa baadaye ni kujenga ukumbi wa kisasa,kuleta huduma jirani ya Supermarket,MinBank na maduka ya vyakula ili kupunguza safari ya kwenda na kurudi mjini ambapo itasaidia sana kuokoa fedha nyingi na muda.

Hata hivyo alisema,Canopies Hoteli inakabiliwa na changamoto chache kati ya hizo ni miundombinu ya barabara,na kuiomba serikali isaidie kujenga barabara ya lami kwani wakati wa masika wageni wanaweza wasiamini kama kuna Hoteli nzuri ya kupumzika.

Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema alisema, Hotel hiyo ni kati ya Hotel zenye hadhi kubwa wilayani Songea ambapo mgeni yoyote anaweza kwenda kwa ajili ya kupumzika.

Alisema,serikali ya wilaya itahakikisha inawaungo mkono wato wote watakaohitaji kwenda Songea kwa ajili ya kuwekeza katika shughuli mbalimbali ikiwamo sekta ya utalii na uwekezaji.

MWISHO.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.