• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI MWAKYEMBE:Uandishi wa habari sio kimbilio la waliofeli

Imewekwa kuanzia tarehe: August 16th, 2020


WAZIRI wa Habari, Sanaa,Utamaduni na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe hivi karibuni amefanya ziara ya kikazi mkoani Ruvuma na kuzungumza na wadau wa Habari katika ukumbi wa Mipango uliopo ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea.

Katika ziara yake Waziri Mwakyembe ametembelea maeneo ya kihistoria yakiwemo Makumbusho ya Taifa ya Majimaji  kutembelea mitambo ya  TBC  Kanda ya ziwa Nyasa,vituo viwili vya redio binafsi vya Jogoo na Key FM na hatimaye kuzungumza na wadau wa habari.

Akizungumza na wadau wa habari,Waziri Mwakyembe amesema kwa muda mrefu wanahabari hapa nchini wamedharauliwa na kukosa haki zao za msingi wanazostahili kupata kama wanahabari.

“Mimi ni mwanahabari mwenzenu, nimekulia humo potelea mbali anayeficha kidonda haponi,Hii tasinia inawezesha nchi na Demokrasia kufanya kazi,imekuwa ni kimbilio la mtu anayefeli duniani,uandishi wa habari siyo wa kupokea makapi’’,amesisitiza Mwakyembe.

Waziri wa Habari ameongeza kuwa Mwandishi ni mwalimu,ni mkalimani,ni mfasili na  mchambuzi wa masuala mbalimbali na kwamba mtu yeyote  ambaye hakidhi vigezo siyo mwandishi wa habari.

Hata hivyo amekiri kuwa hapo awali makosa yalifanyika kwa kuichukulia fani ya uandishi wa habari ni kama makapi ya wanaofeli ambapo mwaka 2016 iliundwa sheria  na kwamba katiba inatambua uandishi wa habari ni taaluma,na kazi ya uandishi wa habari ni hatari na inampasa mwanahabari  kuwekewa Bima,pia aingizwe kwenye mifuko ya hifadhi ya mifuko ya Taifa.

“Sheria ya habari imeundwa  baraza Huru la Habari tulejee kwenye Misimamo tumeunda kamati ya Baraza itakuwa na mamlaka kama mahakama tumegundua bila serikali kuingiza pesa kwenye mifuko yao wengi watashindwa kusoma na kilele chake  mwaka 2021 wanahabari tutakao anza nao kazi 2022 watakuwa wana elimu kuanzia Diploma na Degree’’,alisema.

“Siyo kwamba sina huruma, nina huruma sana,kuna watu wana uzoefu mkubwa lakini hawana Elimu inayotakiwa vijana wote wadogo hakikisheni mnakimbia kwenda kusoma”,alisisitiza Waziri wa Habari.

Katika hatua nyingine Waziri Mwakyembe amekoshwa    shule ya Ruhuwiko Sekondari  iliyopo Songea Mjini kwa kufanya vizuri katika michezo ya UMISETA kitaifa iliyofanyika mwaka 2019 mkoani Mtwara.

Kaimu Afisa Michezo Mkoa wa Ruvuma Anzawe Chaula amesema  mafanikio waliyopata  Kuimarisha Michezo kwa Shule za Msingi na Sekondari  ngazi ya mkoa, ambapo katika mashidano ya UMISETA taifa mwaka 2019  timu ya mpira wa miguu ya mkoa wa Ruvuma iliibuka kinara kitaifa  na kuchangia golikipa bora ambaye aliweza kwenda kushiriki mashindano ya  Afrika Mashariki yaliyofanyika nchini Kenya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi TBC Mhandisi Upendo Mbele amesema usikivu wa  TBC Taifa KATIKA Mkoa wa Ruvuma kwa sasa ni mzuri tukilinganisha na miaka ya 80 ambapo mitambo yake ilichakaa  na usikivu ulikuwa ni hafifu.

Amesema Serikali  kupitia shirika lake la utangazaji  ilimeamua kuweka mitambo mingine mipya ya FM ambapo hadi sasa katika nchi nzima kuna mitambo 67.

Imeandikwa na Aneti Ndonde

Ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.