• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI wa Maji atoa zawadi kwa wananchi waliotunza vyanzo vya maji Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 13th, 2023

WAZIRI wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso ametoa zawadi ya mifuko 150 ya saruji kwa Halmashauri tatu za Mkoa wa Ruvuma na fedha kiasi cha shilingi 500,000  kwa wananchi  waliotunza vyanzo vya maji.

Waziri Aweso alipofanya ziara ya kikazi mkoani Ruvuma aliahidi kutoa zawadi  za saruji mifuko 50  kwa Halmashauri za Nyasa,Halmashauri ya Mbinga mji na Halmashauri ya wilaya ya Mbinga na kutoa fedha shilingi 500,000  kwa Jumuiya moja kati ya sita za watumia maji zilizoundwa mkoani Ruvuma.

Hafla ya kukabidhi zawadi hizo imefanyika kwenye viwanja vya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga  ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ambaye alikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Waziri wa Maji.

Akitoa taarifa ya Bonde hilo kabla ya kukabidhi zawadi hizo, Mkurugenzi wa Bodi Bonde la Maji la Ziwa Nyasa Mhandisi Arice Engalabeth BONDE la Maji la Ziwa Nyasa lina  uwezo wa kutumia maji milimita za ujazo zaidi ya milioni 12 kwa mwaka.

Mhandisi Engalabeth amesema  kati ya milimita hizo za maji,meta  za ujazo milioni 107 ni za maji chini ya ardhi na kwamba bonde la maji la ziwa Nyasa  ni bonde la pili kwa wingi wa maji ya juu ya ardhi kati ya mabonde ya maji tisa yaliyopo nchini.  

 Hata hivyo amesema bonde la maji la ziwa Nyasa ni la mwisho kwa wingi wa maji chini ya ardhi kati ya mabonde tisa yaliyopo nchini na kwamba bonde hilo lina vituo  54 vya kufuatilia mwenendo wa maji   ambapo katika Mkoa wa Ruvuma vituo hivyo vipo katika mito ya Ruhuhu,Ngaka,Lutukira na Lumecha  na katika ziwa Nyasa kuna vituo vitatu vinavyofuatilia wingi wa maji kwa usawa wa ziwa.

“Katika Mkoa wa Ruvuma tumeunda Jumuiya sita  za watumiaji maji,Mkoa wa Ruvuma una mito mingi ambayo inatiririsha maji,hivyo  tunawajibu wa kuhakikisha tunatunza vyanzo vya maji ili viweze kutusaidia kwa maendeleo ya kiuchumi kwa kizazi cha sasa na kijacho’’,alisisitiza Mhandisi Arice.

Amesema Bonde la ziwa Nyasa lina maji mengi ambapo takwimu zilizopo zinaonesha kuwa maji ya bonde la ziwa Nyasa   yakigawanywa kila mtu anaweza kupata meta za ujazo 6644 kwa mwaka ukilinganisha na takwimu za kitaifa ambazo zinaonesha mtu mmoja kwa mwaka anapata meta za ujazo  2005.

Akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi ya mifuko 150 ya saruji na fedha shilingi 500,000 kwa wananchi waliotunza vyanzo vya maji katika wilaya za Mbinga na Nyasa,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas   amewaasa wananchi kuendelea kutunza vyanzo vya maji  kwa kupanda miti rafiki hasa katika kipindi hiki cha mvua.

Amekemea tabia ya baadhi ya wakazi wa Mbinga kukata miti hadi kwenye vilele vya milima na vyanzo vya maji ambapo amemshukuru Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso kwa kutoa zawadi  hizo kwa wananchi waliotunza vizuri vyanzo vya maji katika wilaya hizo.

“Zawadi hizo ziwe kichochea kwa wananchi wengine mkoani Ruvuma ili waweze kutunza mazingira na kuhifadhi vyanzo vya maji,tujifunze kutunza na kuhifadhi kile tulichonacho, kila Halmashauri itekeleze lengo la kupanda miti isiyopungua milioni moja kwa mwaka ili tuwe na uhifadhi endelevu’’,alisisitiza RC Thomas.

Ametoa rai kwa wanahabari kuendelea kuandika Makala za kuhamasisha utunzaji wa mazingira, kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji vilivyopo.

Bonde la maji la ziwa Nyasa linapita katika mikoa ya Mbeya, Ruvuma,Songwe na Njombe.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi  ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.