• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WENYE ULEMAVU Mbinga waiomba serikali kuwapatia watalaam wa lugha za alama

Imewekwa kuanzia tarehe: May 23rd, 2023

CHAMA cha watu wenye walemavu wilayani Mbinga(CHAWATA),kimeiomba serikali kuwapatia wataalam wa lugha za alama waweze kuwasaidia wanapofika katika maeneo ya kutolea huduma na kutoa mchango wao kwenye ujenzi wa Taifa kama ilivyo kwa makundi mengine ya kijamii.

Ombi hilo limetolewa  na katibu wa chama hicho Steven Mateso, wakati akitoa taarifa kuhusu mradi wa ustawi,haki na ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu kwa viongozi wa serikali za mitaa,wadau na jamii wilayani humo.

Alisema kukosekana kwa wataalam hao,kumesababisha kukosa baadhi ya haki zao pindi wanapokwenda katika maeneo ya kutolea huduma za kijamii ikiwemo Hospitali,Mahakama,Polisi na ofisi nyingine za umma kwani inakuwa vigumu kueleweka haraka kwa jamii.

Mateso alitaja changamoto nyingine ni kutopewa nafasi pindi wanapojitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi hasa katika maeneo ya vijijini na kukosa elimu ya ujasiriamali na uzalishaji ili kubuni  miradi ya kuwaingizia kipato.

Kwa mujibu wa Mateso ni kwamba,hata miundombinu katika majengo ya zamani ya kutolea  huduma siyo rafiki kwa walemavu na kutolea mfano ukosefu wa vyoo maalum kwa walemavu.

Alisema,kutoshirikishwa katika vyombo  vya maamuzi ngazi  ya kijiji,kata na Baraza la madiwani vimekuwa kikwazo kwa kamati  za masuala ya watu wenye ulemavu kutekeleza majukumu yake kikamilifu na hivyo kusababisha kundi hilo kubaki nyuma.

Wameiomba serikali kupitia Halmashauri zake,kutenga bajeti ya fedha ili kuiwezesha kamati ya watu wenye ulemavu ziweze kukutana na kujadili masuala muhimu yanayowakabili kama zinavyokutana kamati nyingine.

Aidha alisema,Chawata kimepata ufadhili wa Sh.milioni 33,608,163 kutoka  Foundation for Civil Society ili kutekeleza mradi wa ustawi,haki na ujumuishwaji  wa watu wenye ulemavu katika vyombo vya maamuzi katika kata tatu ambazo ni Muungano,Kitura na Mbangamao.

Alitaja kazi zilizofanyika ni kufanya mafunzo kwa wajumbe 90 wa kamati za vijiji kutoka kata tatu za mradi ambapo jumla ya watu wenye ulemavu 33,wenyeviti wa vijiji 11,watendaji  11,watendaji kata 3 madiwani 3 na wenyeviti wa huduma za jamii 11 na wawakilishi walipata mafunzo husika.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mbinga Aziza Mangosongo alisema,serikali imeanza imeanza kuboresha miundombinu ili kuwawezesha watu wenye ulemavu kufiki kwenye maeneo ya kutolea huduma kwa urahisi na kushiriki  kikamilifu katika ujenzi wa Taifa.

Amewahamasisha watu wenye ulemavu kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi,kujiamini na kushiriki katika kazi mbalimbali za kijamii badala ya kujitenga  na kujinyanyapaa.

Mangosongo,amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri ya wilaya na Mji Mbinga,kuwaalika watu wenye ulemavu kushiriki vikao mbalimbali vya maamuzi ikiwemo baraza la madiwani na kutenga fedha ili kununua mahitaji na vifaa kama mafuta maalum ya ngozi.

Mangosongo,amewaomba wazazi kutowatenga na kuwafungia ndani watu wenye ulemavu bali kuwapa nafasi na haki zao kama elimu,mavazi na huduma nyingine za kijamii.

Mwakilishi wa Chama cha Walemavu Tanzania Said Kombo Kombo (Manara),amewataka watu wenye ulemavu kutokata tamaa au kubaki nyuma,badala yake kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele na kushiriki kazi mbalimbali za ujenzi wa Taifa.

Amewataka kujiamini na kuaminika wanapopata mikopo kutoka katika taasisi za fedha ikiwemo asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri, kwa kurejesha kwa wakati ili kutoa fursa kwa walemavu wengine kukopeshwa badala ya kudhani fedha hizo ni zao.

Amewashauri kuanzisha na kufanya shughuli za kuwaingizia kipato halali kitakachowasaidia kuendesha maisha yao na kuwaondokana na  tabia ya kuomba omba kwa watu wengine katika jamii,jambo ambalo ni aibu kubwa kwao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.